Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Kesi ya Kina Mdee: Chadema yaondoa mapingamizi, shauri kuanza kusikilizwa
Habari za SiasaTangulizi

Kesi ya Kina Mdee: Chadema yaondoa mapingamizi, shauri kuanza kusikilizwa

Spread the love

 

MAHAKAMA Kuu Kanda ya Dar es Salaam imekubali ombi la Wakili wa Chadema, Peter Kibatala, la kuondoa mapingamizi yao dhidi ya kesi ya Halima Mdee na wenzake 18 ya kupinga kuvuliwa uanachama wa chama hicho. Anaripoti Faki Sosi, Dar es Salaam … (endelea).

Mahakama umefanya uamuzi huo leo Jumatano tarehe 29, Juni, 2022 kufuatia maombi ya Kibatala ya kuondosha mapingamizi ya awali waliyowaweka kwenye Hati ya kiapo.

Kibatala ameiomba kuondosha mapingamizi hayo ili kupisha usikilizwaji wa shauri hilo kwa kuwa limefunguliwa mahakamani hapo kwa Hati ya dharura.

Jaji Mustapha Ismail amekubali ombi hilo na kuamua kuondoa mapingamizi hayo kabla ya shauri la msingi kuendelea kusikilizwa ambapo amesema kuwa amri ya zuio itaendelea mpaka shauri la msingi litakapofika mwisho.

“Baada ya kusikiliza hoja za Mawakili nimeamua Hati ya mapingamizi ya awali inaondolewa mapingamizi yote hayatataendelea”

Pia Jaji Mustapha amesema kuwa amri ya itaendelea mpaka mwisho wa shauri la msingi.
Wakati huo huo kolamu ya Mawakili imejitambulisha mbele ya Jaji kwa ajili ya kuendelea na shauri hilo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!