Friday , 29 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Kesi kupinga wakurugenzi kusimamia chaguzi; serikali yakwama kortini
Habari Mchanganyiko

Kesi kupinga wakurugenzi kusimamia chaguzi; serikali yakwama kortini

Mahakama Kuu ya Tanzania
Spread the love

MAHAKAMA Kuu Kanda ya Dar es Salaam imetupilia mbali pingamizi la serikali kwenye shauri la kupinga utaratibu wa kuteuwa Mkurugenzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) na Wakurugenzi wa Manispaa na Halmashauri kuwa wasimamaizi wa uchaguzi. Anaripoti Faki Sosi…(endelea).

Kesi hiyo iliyofunguliwa na  Mwanaharakati Bob Chacha Wangwe ambapo leo tarehe 13 Februari 2019, mahakama imeelezea kuwa, waombaji wanahaki ya kisheria kufungua shauri hilo.

Awali serikali ilitaka kesi hiyo itupiliwe mbali kwa sababu, waombaji hawakustahili kufika mahakamani na badala yake kwenda kulalamika kwenye utawala wa tume.

Tarehe ya kuendelea kusikilizwa kesi hiyo itatajwa saa nane mchana baada ya mahakama kurejea tena.

Bob Chacha Wange kupitia wakiliwa wake Fatma Karume amemshtaki Mwanasheria  Mkuu wa Serikali (AG), Tume ya Uchaguzi ya Taifa (NEC)  na mkurugenzi  wake.

Bob Chacha Wangwe amefungua kesi hiyo kikatiba baada ya kuamini kuwepo kwa udhaifu wa tume hiyo. Amedai kuwa, tume hiyo inaongozwa na makada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) ambao hawaendishi uchaguzi wa haki.

Bob Chacha Wange ni mtoto wa marehemu Chacha Wangwe aliyewahi kuwa Mbunghe wa Tarime mjini (Chadema).

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mtandao watetezi wa haki za mazingira Tanzania waundwa

Spread the loveMTANDAO wa watetezi wa haki za mazingira nchini Tanzania, umeundwa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

error: Content is protected !!