Friday , 19 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Kenyatta, Kagame waitaka M23 kusitisha mapigano na kujiondoa DRC
Kimataifa

Kenyatta, Kagame waitaka M23 kusitisha mapigano na kujiondoa DRC

Spread the love

 

JUMUIYA ya Afrika Mashariki imesema Rais wa zamani wa Kenya Uhuru Kenyatta na Rais wa Rwanda Paul Kagame wamekubaliana juu ya haja ya waasi wa M23 kusitisha mapigano na kujiondoa katika maeneo ya mashariki mwa Kongo.

Taarifa ya Jumuiya hiyo imeongeza kuwa Kagame amekubali pia kumsaidia Kenyatta kuwahimiza waasi wa M23 kutekeleza matakwa hayo.

Mbinu za kufanikisha hatua hiyo zitajadiliwa wakati wa duru ya pili ya mazungumzo katika mji mkuu wa Angola Luanda wiki ijayo.

Naibu msemaji wa Rais wa Kongo ameliambia shirika la habari la Reuters kuwa hatua hii inatia moyo kuona Paul Kagame ametambua kuwa anaweza kuwashawishi M23, lakini amesema wanasubiri kuona kitakachotokea katika uwanja wa vita.

Makabiliano ya hivi karibuni kati ya waasi wa M23 na vikosi vya Kongo yamepelekea maelfu ya watu kuyahama makazi yao.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!