Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Kenyatta: Dunia itatuheshimu EAC tukipata maendeleo kwa umoja wetu
Habari za SiasaTangulizi

Kenyatta: Dunia itatuheshimu EAC tukipata maendeleo kwa umoja wetu

Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki
Spread the love

 

RAIS wa Jamhuri ya Kenya na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Uhuru Kenyatta amesema wananchi wa Jumuiya hiyo wakiungana na kushirikiana katika maendeleo dunia itawaheshimu. Anaripoti Mwandishi Wetu, Arusha … (endelea).

Kenyatta amaeyasema hayo leo Ijumaa tarehe 22 Julai, 2022, jijini Arusha wakati wa uzinduzi wa kilomita 14 za barabara ya Arusha-Moshi-Holili na barabara ya mchepuko ya Arusha kilomita 42.4.

Rais huyo ambaye amebakisha siku chache madarakani, amesema endapo nchi hizo zitashairikiana hakuna jambo watakaloshindwa kulifanya na kuwa nchi za mfano Afrika na duniani.

Amesema maendeleo hayo yatakuja endapo wananchi watawaunga mkono viongozi wao akitolea mfano wa namna Watanzania walivyomuunga mkono Rais Samia Suluhu Hassan wakati akiipokea wadhifa huo wakati wa majonzo na huzuni.

“Mama (Rais Samia) alikuja akashikilia, akawa mjasiri, mchapakazi na kazi mnaiona leo inaendelea na inasonga mbele, kwahivyo ni ishara kuwa tukiwaunga viongozi wetu mkono, tukishikirikiana pamoja kama wananchi wa EAC hakuna jambo linatushinda, tunaweza kubadilisha nchi zetu ziwe nchi viongozi sio tu kwa Afrika bali dunia na tuheshimiwe na dunia kwasababu ya umoja wetu na maendeleo ambayo tunayatekeleza kwasababu ya huo umoja,” amesema Kenyatta.

“Ningependa kuchukua nafasi hii kumshukuru dada yetu mama Rais Samia Suluhu Hassan kwasababu alikuja kuchukua uskani wa nchi ya Tanzania wakati wa majonzi na huzuni…watu walikuwa wanahofu itakuwaje, lakini alituonyesha kwamba msemo wa Kiswahili kweli una maana, Usimwone simba amenyeshewa ifikirie ni paka,” amesema.

Katika hatua nyingine Kenyatta alipongeza jitihada zinazofanywa na nchi hizo kuboresha miundombinu ya usafirishaji inayoziunganisha.

Kenyatta amesema “umuhimu wa miundombinu hauwezi kupuuzwa kwasababu ndiyo msingi wa maendeleo yote, tukiwa kwanza na amani na wananchi wetu wanaishi kwa amani, ya pili ni miradi kama hii kusaidia wananchi kusafiri kupeleka mizigo yao na kujumuika na wenzao wa nchi jirani kwa njia rahisi.

Amesema endapo wananchi wataweza kutembea kutoka Arusha-Holili-Taveta-Voi hadi Mombasa itasaidia wananchi kuwa karibu zaidi na kusaidia biashara ziweze kuimarika, “usafirishaji wa mizigo utakuwa rahisi, nyanya, mboga, mahindi na bidhaa tofauti tofauti zitakuwa zinatembea na kuingia kwenye soko kwetu kule Nairobi kwa njia rahisi,” amesema na kuongeza “na hiyo ni utajiri kwa wakulima Watanzania na wafanyabiashara wa Kenya na njia ya kumaliza umasikini katika nchi zetu.

“Leo ni siku ya furaha tukiungana na viongozi wenzetu wa Afrika Mashariki kuzindua barabara ambayo itakuwa na manufaa kwa mji huu ambao ni moyo wa Afrika mashariki, itapanua miji na kupunguza msongamano na kutuunganisha nchi za Afrika Mashariki,” amesema Kenyatta.

1 Comment

  • SHAMBA LA BIBI
    Kenya mlivunja Jumuiya ya Afrika Mashariki mwaka 1977. Tukafunga mpaka mkaenda kuomba msaada wa chakula Marekani.
    Tunataka uwiano sawa…siyo nyinyi mnaleta biashara 500 na sisi mnatupa 50.
    Kwanza, hizi biashara siyo zenu. Mnatumiwa na wafanyabiashara haramu wa nchi zingine kusajili kampuni zao kwenu na kuja kutuibia.
    Tanzanite na dhahabu mlizonazo ni za Hao wageni, siyo nyinyi.
    Viazi, vitunguu, mchele,, mahindi, sukari na vitu vingine mvilipie kwa uwazi na siyo magendo.
    Tusiendelee kuwa shamba lao la bibi!

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!