Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Kenya Airway yapata hasara ya mabilioni
Kimataifa

Kenya Airway yapata hasara ya mabilioni

Ndege ya Shirika la Ndege la Kenya
Spread the love

SHIRIKA la Ndege la Kenya limetangaza kupata hasara ya kiasi cha Shilingi za Kenya 7. 59 Bil (Takriban 151 Bil za Tanzania ) kwa mwaka wa 2018. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).

Taarifa ya hasara hiyo ilitolewa tarehe 29 Aprili 2019 na jarida maarufu nchini Kenya la masuala ya uchumi na fedha la Business Daily kupitia ukurasa wake wa mtandao wa Twitter. 

Shirika la Ndege la Kenya limesema, hasara hiyo imetokana na ukubwa wa gharama za uendeshaji ikiwemo kupanda kwa bei ya mafuta na mishahara ya watumishi wa shirika hilo.

Aidha, hasara hiyo ni pungufu ukilinganisha na hasara iliyopata Shirika la Ndege la Kenya kwa mwaka wa fedha wa 2017 ambapo ilikuwa Ksh. 9.44 Bil.

Hata hivyo, shirika hilo limetangaza ongezeko la mapato ya kiasi cha Ksh. 114.45 bilioni ikilinganishwa na mwaka 2017 ambapo yalikuwa ni Ksh. 106.2 bilioni.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoKimataifa

Zuma akataliwa kugombea urais

Spread the loveTUME Huru ya Uchaguzi Afrika Kusini (IEC) imemwondoa rais wa...

KimataifaTangulizi

Zuma akataliwa kugombea urais

Spread the love  TUME Huru ya Uchaguzi Afrika Kusini (IEC) imemwondoa rais...

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaKimataifa

Faye aahidi kuongoza kwa unyenyekevu, wagombea wenzie wakubali yaishe

Spread the loveMgombea wa upinzani Senegal, Bassirou Diomaye Faye anajiandaa kuwa rais...

error: Content is protected !!