Tuesday , 3 October 2023
Home Kitengo Habari Kimataifa Kenya Airway yapata hasara ya mabilioni
Kimataifa

Kenya Airway yapata hasara ya mabilioni

Ndege ya Shirika la Ndege la Kenya
Spread the love

SHIRIKA la Ndege la Kenya limetangaza kupata hasara ya kiasi cha Shilingi za Kenya 7. 59 Bil (Takriban 151 Bil za Tanzania ) kwa mwaka wa 2018. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).

Taarifa ya hasara hiyo ilitolewa tarehe 29 Aprili 2019 na jarida maarufu nchini Kenya la masuala ya uchumi na fedha la Business Daily kupitia ukurasa wake wa mtandao wa Twitter. 

Shirika la Ndege la Kenya limesema, hasara hiyo imetokana na ukubwa wa gharama za uendeshaji ikiwemo kupanda kwa bei ya mafuta na mishahara ya watumishi wa shirika hilo.

Aidha, hasara hiyo ni pungufu ukilinganisha na hasara iliyopata Shirika la Ndege la Kenya kwa mwaka wa fedha wa 2017 ambapo ilikuwa Ksh. 9.44 Bil.

Hata hivyo, shirika hilo limetangaza ongezeko la mapato ya kiasi cha Ksh. 114.45 bilioni ikilinganishwa na mwaka 2017 ambapo yalikuwa ni Ksh. 106.2 bilioni.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Kimataifa

Urusi yafungua milango kwa nchi za Afrika

Spread the loveSERIKALI ya Urusi imefungua milango ya ushirikiano wa kiuchumi, kijamii...

Kimataifa

Wadukuzi wa Kichana waiba barua pepe 60,000 za Serikali ya Marekani

Spread the loveWADUKUZI wa kichana wamedukua barua pepe 60000 serikali ya Marekani...

Kimataifa

Putin aita vikundi vya kujitolea vita ya Ukraine

Spread the loveRAIS wa Urusi, Vladimir Putin, amefungua milango ya ushirikiano kwa...

Kimataifa

Mlipuko wa bomu waua 50 katika sherehe za Maulidi ya Mtume

Spread the loveWATU takribani 50 wamefariki dunia huku wengine 50 wakijeruhiwa katika...

error: Content is protected !!