Thursday , 23 March 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Kelele zatawala Sabaya, wenzake wakifikishwa mahakamani
Habari za Siasa

Kelele zatawala Sabaya, wenzake wakifikishwa mahakamani

Lengai Ole Sabaya, aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai, akiwasili mahakamani
Spread the love

 

LENGAI Ole Sabaya, aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai, Mkoa wa Kilimanjaro na wenzake watano, wamefikishwa katika Mahakama mkoani Arusha. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Sabaya na wenzake watano, wamefikishwa tena mahakama leo Ijumaa, tarehe 18 Juni 2021.

Ni baada ya kufikishwa kwa mara ya kwanza, tarehe 4 Juni 2021 na kusomewa mashtaka sita kwa mahakimu wawili tofauti.

Mara baada ya gari la magereza kuwasili mahakamani hapo, umati wa watu walikuwa wamejitokeza kushuhudia kinachoendelea.

Wenzake watano ni; Sylivesta Nyegu, Wadson Stanley, Enock Togolan, John Odemba na Daniel Mbura.

Sabaya na wenzake, wanakabiliwa na mashtaka ya; unyang’anyi kwa kutumia silaha, kushiriki vitendo vya rushwa , kutakatisha fedha, uhujumu uchumi na kuongoza magenge ya uhalifu.

Kelele za baadhi ya wananchi waliokuwepo mahakamani zilisikika huku wengine wakisema ‘mwizi, mwizi, mwizi’

Tofauti na walivyofikishwa mara ya kwanza, leo Ijumaa, Sabaya alikuwa kavalia kaunda suti huku akiwa ameshikilia kitabu mkononi.

Wakazi wa Arusha wakiwa nje ya mahakama wakifuatilia kesi hiyo

Endelea kufuatilia MwanaHALISI na MwanaHALISI TV kwa habari na taarifa mbalimbali ya kitakachojili mahakamani

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Rais Samia aagiza iundwe kamati ya pamoja ya Mawaziri mradi wa BBT

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amewaagiza mawaziri kuunda kamati...

Habari za Siasa

Rais Samia apangua makatibu tawala mikoa, ateua Kamishna DCEA

Spread the loveALIYEKUWA Kamishna wa Mamlaka ya Kudhibiti Dawa za Kulevya, Gerald...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

M/kiti bodi ya wadhamini Chadema afariki dunia

Spread the loveMWENYEKITI wa Bodi ya Wadhamini ya Chama cha Demokrasia na...

Habari za Siasa

Zitto: Nikifa Ado atavaa viatu vyangu

Spread the love  KIONGOZI Mkuu wa Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe...

error: Content is protected !!