Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Kauli yake dhidi ya Magufuli, Mdee kupanda Kisutu tena
Habari za Siasa

Kauli yake dhidi ya Magufuli, Mdee kupanda Kisutu tena

Spread the love

HALIMA Mdee, Mbunge wa Kawe, jijini Dar es Salaam leo anapanda tena kizimbani kuendelea na shauri lake kuhusu kutoa lugha chafu dhidi ya Rais John Magufuli alilofunguliwa mwaka 2017. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Shauri hilo lipo mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu Thomas Simba katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu ambapo tayari upande wa mashataka umetoa ushahidi wake akiwemo Mkuu wa Kituo cha Urafiki, Mrakibu wa Polisi (SP) Batseba Kasanga.

Katika shauri hilo Mdee akiwa katika Makao Makuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) tarehe 3 Julai 2017 anadaiwa kutamka maneno machafu dhidi ya Rais Magufuli.

Mdee anaiwa kutamka “anaongea hovyohovyo, anatakiwa afungwe breki” ambapo kwa mara ya kwanza alifikishwa mahakamani hapo tarehe 10 Julai 2017.

Mahakama ya Kisutu leo Alhamis 7 Februari 2019 itaendele kusikiliza ushahidi kwenye kesi hiyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Chadema yamtaka Rais Samia aunde tume kuchunguza mauaji mgodi wa Barick

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, ameombwa aunde tume huru kwa...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

error: Content is protected !!