Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari Katibu Tawala Arusha afariki ajalini
HabariTangulizi

Katibu Tawala Arusha afariki ajalini

Spread the love

 

KATIBU Tawala Mkoa wa Arusha (RAS), Richard Kwitega, amefariki dunia leo Jumatano saa 9:30 alasiri, tarehe 3 Februari 2021, katika ajali ya gari eneo la Mdori, Wilaya ya Babati, mkoani Manyara. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea)

Ajali hiyo, imehusisha gari lake na basi la abiria, ambapo Kwitega alikuwa anakwenda jijini Dodoma kikazi.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-Tawaza za Mikoa na Serikali za MItaa (Tamisemi), Selemani Jafo amesema, mareemu Kwitenga, aliteuliwa na Rais John Magufuli kuwa RAS, tarehe 25 Aprili 2016.

Amesema, kabla ya uteuzi huo, aliwahi kufanya kazi katika mikoa mbalimbali nchini na “Serikali inatambua na itaendelea kuenzi mchango wa marehemu Richard Nkingwa Kwitega katika ujenzi wa Taifa letu.”

Waziri Jafo amesema, taarifa zaidi kuhusu taratibu za mazishi zitaendelea kutolewa na uongozi wa mkoa wa Arusha.

Mapema leo asubuhi, Kwitenga alifungua mkutano mkoani humo na kuwaaga washiriki kwamba anakwenda Dodoma kikazi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Zuma akataliwa kugombea urais

Spread the love  TUME Huru ya Uchaguzi Afrika Kusini (IEC) imemwondoa rais...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!