KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Daniel Chongolo, ametoa wito kwa vijana wanaohitimu vyuo vikuu, wafanye shughuli nyingine za kujitafutia kipato ambazo ziko nje ya taaluma walizosomea. Anaripoti Mwandishi Wetu, Singida … (endelea).
Chongolo ametoa ushauri huo leo tarehe 27 Februari 2023, katika ziara yake ya kikazi mkoani Singida.
Mbali na ushauri huo kwa wahitimu wa vyuo vikuu, Chongolo amewataka wazazi na walezi kuwapeleka watoto wao katika vyuo vya elimu na ufundi stadi (VETA), kwa ajili ya kujiongezea ujuzi wa kujiari, badala ya kuwaacha vijiweni.
“Vijana wengi wakishamaliza vyuo akiwa na digrii ya ualimu, haamini kama anaweza kuwa na uwezo wa kufanya kitu kingine nje ya taaluma aliyonayo. Tunajenga vyuo vya VETA kote nchini lengo kusogeza elimu ya ujuzi karibu na wananchi, pelekeni vijana waende wakasome na kupata ujuzi kwani utawapa uhakika wa kujiajiri na kujitafutia shilingi,” amesema Chongolo.
Aidha, Chongolo amewataka viongozi wa Serikali ngazi ya wilaya, kuanzisha program za kuwapelekea VETA vijana walioko katika maeneo yao.
@THINK/Dedication/Remember”@ EMPLOY/US THEM ALL – ALL TANZANIAN HAS JOB TO DO
In 2021, the unemployment rate in Tanzania remained nearly unchanged at around 32.74 percent. With a decline of 0.04 percentage points, there is no significant change to 2020. Over the observed period, the unemployment rate has been subject to fluctuation.