Saturday , 20 April 2024
Habari za Siasa

Katibu Chadema auawa

Sweetbert Njewike, Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani Singida
Spread the love

ALEX Jonas, Katibu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Manyoni Mashariki mkoani Singida, ameuawa. Anaripoti Mwandishi Wetu, Singida … (endelea).

Taarifa zaidi zinaeleza, Jonas ameuawa usiku wa kuamkia jana tarehe 25 Februari 2020, na mpaka sasa watu waliofanya tukio hilo, hawajajulikana.

Sweetbert Njewike, Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani Singida akizungumza na MwanaHalisi Online kwa njia ya simu kuhusu mauaji hayo, amesema Jeshi la Polisi linayo taarifa hiyo na kwamba linafuatilia.

Kamanda Njewike amesema, Mkuu wa Polisi Wilaya ya Manyoni (OCD), anafuatilia tukio hilo, na kwamba atatoa taarifa rasmi pindi ufuatiliaji huo utakapokamilika.

“Nimesikia kuna mtu ameuawa lakini sijajua kama ni katibu wa chadema, OCD Manyoni anafuatilia tutajua kama ni huyo. Taarifa rasmi tutatoa baadaye, nasubiri kwanza taarifa kutoka kwa OCD wa wilaya hiyo,” amesema Kamanda Njewike.

Kwa mujibu wa Chadema leo tarehe 26 Februari 2020, mwili wa Jonas ulikutwa eneo la Mwembeni Manyoni Mjini, ukiwa umekatwa na mapanga maeneo mbalimbali ya mwili hasa kichwani na mikononi.

Chama hicho kimesema, kinafuatilia kwa undani kuhusu tukio hilo, huku kikilaani mauaji hayo.

“Tumepata taarifa za kushtua na kusikitisha sana za mauaji ya katibu wa Chadema Manyoni Mashariki ndugu Alex Jonas yaliyotokea usiku wa kuamkia jana, Mwembeni Manyoni Mjini. Chama kinafuatilia kujua kilichotokea kisha tutatoa taarifa juu ya tukio hilo,” imeeleza taarifa ya Chadema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

Habari za Siasa

Wabunge waikalia kooni TAKUKURU Bungeni

Spread the love  BAADHI ya wabunge wamelia na changamoto za utendaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

error: Content is protected !!