FREEMAN Mbowe, Mwenyekiti wa Chama Kikuu cha Upinzani, Tanzania- Chadema amesema, Jumamosi zote kuanzia kesho, tarehe 12 Juni 2021, atakuwa akivaa sare za chama hicho hadi nchini hiyo ipate Katiba Mpya. Anaripoti Nasra Bakari, DMC … (endelea).
Mchakato wa Katiba Mpya, uliishia kwa Katiba Pendekezwa ambapo, Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), tarehe 2 Aprili 2015, ilitangaza kuahirishwa kwa kura ya maoni ya katiba hiyo.
Kura hiyo ya maoni, ilikuwa ifanyike tarehe 30 Aprili 2015, lakini iliahirishwa kutokana na kutokamilika kwa uandikishaji wa Daftari la kudumu la wapiga kura kwa kutumia teknolojia ya Biometric Voters Registration (BVR).
Leo Ijumaa, tarehe 11 Juni 2021, Mbowe ametumia ukurasa wake wa Twitter kuitangaza Jumamosi kuwa siku ya mavazi ya chama hicho.
“Kesho & kila J’mosi nitavaa sare za chama chetu Chadema hadi TZ ipate Katiba Mpya.”
“Azimio hili limependekezwa & kuungwa mkono & Vikao & Mikutano yote inayoendelea nchini. Wanachadema wote tuungane, tutambuane, tukilinde Chama & tutetee Uhuru na Haki popote tulipo. Umoja ni nguvu!” ameandika Mbowe aliyeanza kukiongoza chama hicho tangu mwaka 2004.
Asante ndugu mbowe kuvaa jezi sio ushind fikiria mbinu za kuleta ushind wanacho itaji wananchi ni mafaniko yenye maishA bora ndio maana ccm katika kampeni zake haikuzumzia swala la katiba ccm imazumzia maitaji ya wananchi na ikaidi itatimiza kwa vitendo maitaji yenye kuleta mafaniko na maendeleo ndio maana watanzania wakichagua ccm kwaio mbowe shida ya watanzania sio katiba