Thursday , 28 March 2024
Home Kitengo Michezo Karia: Mwakalebela alistahili adhabu kali zaidi
Michezo

Karia: Mwakalebela alistahili adhabu kali zaidi

Frederick Mwakalebela, Makamu Mwenyekiti wa Yanga
Spread the love

 

RAIS wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Wallace Karia amesema, Makamu Mwenyekiti wa klabu ya Yanga, Fedrick Mwakalebela alipaswa kupewa adhabu kali kutokana na nyaraka zenye kanuni mbalimbali, alizisaini yeye akiwa katibu mkuu wa shirikisho hilo. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Karia ameyasema hayo leo Jumatatu, tarehe 3 Mei 2021, kwenye mahojiano yake na kituo cha radio cha E-Fm kwenye kipindi cha Joto la Asubuhi na kupigilia msumali kuwa adhabu za kufungia baadhi ya watu kwenye familia ya mpira zinasaidia.

Wakati akielezea sakata la kufungia miaka mitano kwa kiongozi huyo wa klabu ya Yanga, Karia amesema, Mwakalebela ndiye aliyepitisha na kusaini nyaraka zenye sheria hizo wakati akiwa katibu mkuu wa TFF chini ya utawala wa Leodger Tenga hivyo alipaswa kupewa adhabu kali zaidi hii.

Walace Karia, Rais wa TFF

“Mwakalebelea hizi nyaraka zenye kanuni mbalimbali, kazitengeneza yeye na ndio aliyesaini pamoja na Tenga na anajua, kwa hiyo mtu wa namna hii anatakiwa apate adhabu kali zaidi” amesema Karia

Makamu Mwenyekiti huyo wa Yanga, amefungiwa kujihusisha na soka katika kipindi cha miaka mitano na kamati ya maadili ya TFF mara baada ya kushindwa kuthibitisha tuhuma alizozitoa juu ya shirikisho hilo na bodi ya Ligi ya kuwa wanaihujumu klabu ya Yanga.

Taarifa ya kufungiwa kwa Mwakalebela, iliyotolewa na TFF tarehe 2 Aprili 2021, ilieleza adhabu ya kumfungia miaka mitano, kiongozi hiyo imetolewa kwa kuzingatia kifungu cha 73(4) cha kanuni za maadili toleo la 2013 mara baada ya kushindwa kuthibitisha madai hayo.

Mwakalebela alitoa tuhuma hizo tarehe 19 Februari 2021, alipofanya mkutano na waandishi wa habari makao makuu ya klabu ya Yanga na kutoa madai hayo.

Katika hatua nyingine, Karia aliendelea amesema, wataendelea kuwafungia viongozi au mtu yoyote aatakafanya kosa na kwenda kinyume na kanuni pamoja na sheria zilizopo.

“Mkitaka tufanye mnavyotaka ninyi tutarudi kule, itakuwa utawala wa kambale kila mtu ana ndefu mkiona nimewaonea nendeni mkanishtaki maadili,” amesema

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Makala & UchambuziMichezo

TFF kuamua hatima ya Amrouche

Spread the loveHATIMA ya Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Adel Amrouche kuendelea...

Habari za SiasaMichezo

Matinyi: Dk. Ndumbaro alifanya utani ukaguzi mechi za Yanga, Simba

Spread the loveMsemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi amesema kauli iliyotolewa na...

Michezo

Gethsemane Group Kinondoni (GGK) waachia video ya Bwana Wastahili

Spread the loveWAIMBAJI maarufu nchini kutoka Gethsemane Group Kinondoni (GGK)SDA wameachia video...

BiasharaMichezo

Gamondi kocha bora mwezi Februari, NBC yamjaza manoti

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambae ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!