Friday , 19 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Karantini ya Covid kwa wasafiri China mwisho Januari
Kimataifa

Karantini ya Covid kwa wasafiri China mwisho Januari

Spread the love

 

CHINA itaondoa karantini kwa wasafiri kuanzia tarehe 8 Januari, maafisa wamesema, kuashiria mabadiliko makubwa ya mwisho kutoka kwa sera ya sifuri ya Uvik0-19 ya nchi hiyo. Yanaripoti Mashirika ya Kimataifa … (endelea)

Baada ya miaka mitatu ya mipaka iliyofungwa, hii itafungua tena nchi kwa wale walio na safari za kazi na kusoma, au wanaotaka kutembelea familia.

Hatua hii inakuja wakati ambao China inapambana na kuenea kwa virusi hivyo kwa sababu ya vizuizi kuondolewa.

Ripoti zinasema hospitali zimezidiwa na wazee wanakufa.

Idadi ya kweli – hesabu za kila siku na vifo – haijulikani kwa sasa kwa sababu maafisa wameacha kutoa takwimu ya Covid.

Beijing ilikuwa imeripoti takriban maambukizo mapya 4,000 ya Covid kila siku wiki iliyopita na vifo vichache.

Siku ya Jumapili ilisema itaacha kuchapisha nambari za kesi kabisa.

Lakini kampuni ya takwimu ya afya ya Uingereza Airfinity ilikadiria China ilikuwa ikipata maambukizi zaidi ya milioni moja na vifo 5,000 kwa siku, kulingana na Reuters.

Sera inayoitwa “zero-Covid” ilidhoofisha uchumi na kuwafanya raia kuchoka kwa vizuizi na vipimo vya mara kwa mara.

Chuki dhidi ya sera hiyo ililipuka na kwa kufanyika maandamano adimu ya umma dhidi ya Rais Xi Jinping mnamo Novemba, ambayo yalisababisha viongozi kutupilia mbali sheria za Covid wiki chache baadaye.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!