MABEKI wa klabu ya Simba Shomary Kapombe na Henock Inonga sambamba na kiungo mshambuliaji wa klabu hiyo Peter Banda wamewekwa kwenye kinyang’anyiro cha kuwania tuzo ya mchezaji bora wa mashabiki wa klabu hiyo kwa mwezi Februari. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea)
Tuzo hiyo ya mashabiki (Emirates Aluminium ACP Simba Fans) hutolewa kila mwezi kwa mchezaji ambaye amefanya vizuri kwenye michezo husika.
Kwa upande wa Kapombe ameingia kwenye tatu bora mara baada ya kucheza michezo minne ndani ya mwezi Februari, huku akifunga bao moja na kuhusika katika mabao mengine manne.
Peter Banda ndani ya mwezi huo huo alicheza michezo minne, na kufunga bao mmoja kama ilivyo kwa Kapombe na kuhusika katika mabao manne mengine yaliyofungwa kwenye michezo hiyo.
Aidha kwa upande wa beki kisiki wa klabu hiyo Ingona yeye amekuwa na msimu mzuri toka alipojiunga na mabingwa hao wa Ligi Kuu Tanzania Bara kwenye dirisha kubwa la usajili na kucheza michezo mingi ulilinganisha na baadhi ya wachezaji waliosajili kwa msimu huu.
Inonga katika mwezi Februari amecheza michezo zote sita za mwezi Februari akiwa sehemu ya kikosi cha kwanza cha timu hiyo.
Ikumbukwe mshindi wa tuzo hiyo atakabidhiwa kiasi cha Shilingi 2,000,000 na wadhamini wa tuzo hiyo, kampuni ya Emirates Aluminium ACP.
Leave a comment