Tuesday , 5 December 2023
Home Kitengo Habari Kimataifa Kanye West aanza kampeni za urais Marekani
Kimataifa

Kanye West aanza kampeni za urais Marekani

Kanye West
Spread the love

KANYE West, mwamauziki wa mtindo wa kufoka foka, ameanza safari ya kutaka kuwa rais wa Marekani kwenye uchaguzi mkuu mwaka huu. Inaripoti mitandao ya kimataifa … (endelea).

Tayari amefanya mikutano katika miji ya Charleston na South Carolina. Hata hivyo, mikutao yake inaelezwa kutokuwa na msisimko kama mgombea urais. West (43) anawania urais kupitia chama chake cha Birthday Party.

Hata hivyo, mwanamuziki huyo amekumbana na kejeli kutoka kwa wakazi wa miji mbalimbali ya nchi hiyo, kwamba anachokifanya West ni kutaka umaarufu.

Katika mkutano wa Charleston, hakuonesha kuwa na maandalizi ya kufanya mkutano huo lakini wakati anaanza kampeni zake, kwenye ukurasa wake wa Twitter, ulionesha nyimbo za albamu anayotaka kutoa, jambo ambalo limeongeza maswali.

Akiwa amenyoa nywele sehemu ya nyuma ya kichwa chake, alizungumza na watu waliomzunguka bila kutumia kipaza sauti.

Mara kadhaa alikuwa akiwataka watu watulie pale alipoulizwa maswali ili asililize kutokana na kuwepo kwa msongamano wa watu, bila kuwepo kwa teknolojia yoyote ambayo ingerahisisha mawasiliano.

Moja ya sera zake ni kuhusu utoaji wa mimba, alimwaga chozi akisema mama yake nusura amtoe uhai akiwa tumboni mwake. Hata hivyo, amesema utoaji huo uendelee lakini sheria zifuatwe.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Kimataifa

Muandamanaji ajichoma moto akipinga vita Palestina, Israel

Spread the loveMUANDAMANAJI moja ambaye hajafahamika jina, yuko mahututi hospitalini akitetea uhai...

Kimataifa

Urusi kuongeza wanajeshi ikijihami dhidi ya NATO

Spread the loveSERIKALI ya Urusi iko katika mpango wa kuongeza wanajeshi wake,...

Kimataifa

Israel yarejesha mashambulizi Gaza ikilaumu Hamas kukiuka makubaliano

Spread the loveJESHI la Israel, limerejesha mashambulizi katika ukanda wa Gaza, baada...

Kimataifa

Papa Francis kumfukuza Kardinali anayepinga mageuzi Kanisa Katoliki

Spread the loveKIONGOZI wa Kanisa Katoliki duniani, Papa Francis, anadaiwa kupanga kumfumkuza...

error: Content is protected !!