Friday , 19 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Kanye West aanza kampeni za urais Marekani
Kimataifa

Kanye West aanza kampeni za urais Marekani

Kanye West
Spread the love

KANYE West, mwamauziki wa mtindo wa kufoka foka, ameanza safari ya kutaka kuwa rais wa Marekani kwenye uchaguzi mkuu mwaka huu. Inaripoti mitandao ya kimataifa … (endelea).

Tayari amefanya mikutano katika miji ya Charleston na South Carolina. Hata hivyo, mikutao yake inaelezwa kutokuwa na msisimko kama mgombea urais. West (43) anawania urais kupitia chama chake cha Birthday Party.

Hata hivyo, mwanamuziki huyo amekumbana na kejeli kutoka kwa wakazi wa miji mbalimbali ya nchi hiyo, kwamba anachokifanya West ni kutaka umaarufu.

Katika mkutano wa Charleston, hakuonesha kuwa na maandalizi ya kufanya mkutano huo lakini wakati anaanza kampeni zake, kwenye ukurasa wake wa Twitter, ulionesha nyimbo za albamu anayotaka kutoa, jambo ambalo limeongeza maswali.

Akiwa amenyoa nywele sehemu ya nyuma ya kichwa chake, alizungumza na watu waliomzunguka bila kutumia kipaza sauti.

Mara kadhaa alikuwa akiwataka watu watulie pale alipoulizwa maswali ili asililize kutokana na kuwepo kwa msongamano wa watu, bila kuwepo kwa teknolojia yoyote ambayo ingerahisisha mawasiliano.

Moja ya sera zake ni kuhusu utoaji wa mimba, alimwaga chozi akisema mama yake nusura amtoe uhai akiwa tumboni mwake. Hata hivyo, amesema utoaji huo uendelee lakini sheria zifuatwe.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!