Friday , 19 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Kansela mpya Ujerumani ahutubia Bunge, atoa mwekeleo
Kimataifa

Kansela mpya Ujerumani ahutubia Bunge, atoa mwekeleo

Olaf Scholz
Spread the love

 

KANSELA mpya wa Ujerumani, Olaf Scholz amelihutubia kwa mara ya kwanza bunge leo Jumatano, tarehe 15 Desemba 2021 na kuelezea miongozo ya miaka minne ya serikali yake iliyoingia madarakani wiki iliyopita. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Kansela Scholz ameliambia bunge hilo kwamba serikali yake itaipa nguvu zaidi Ujerumani na kujenga mustakabali wenye uhakika.

Aidha, Scholz amesema, kipaumbele chake ni kujenga Umoja wa Ulaya wenye mshikamano zaidi na kupambana na migawanyiko ambayo imekuwa ikiuathiri Umoja huo.

wa muungano wa kihafidhina CDU/CSU, Ralph Brinkhaus, amesema haoni dalili nyingi za maendeleo kwenye serikali ya muungano inayoongozwa na Scholz.

Chama cha siasa za wastani cha mrengo wa kushoto cha Social Democrats, kile cha kijani na kinachoegemea biashara cha FDP vilitia saini mkataba wa muungano mwanzoni mwa mwezi Disemba, takriban wiki 10 baada ya uchaguzi.

Scholz alichaguliwa na bunge kama Kansela wa tisa Ujerumani na kuchukua nafasi ya Angela Merkel baada ya miaka 16 madarakani.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!