Saturday , 20 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Kanisa Katoliki Geita lililonajisiwa lafungwa kwa muda
Habari Mchanganyiko

Kanisa Katoliki Geita lililonajisiwa lafungwa kwa muda

Spread the love

 

KANISA Kuu la Kiaskofu la Jimbo Katoliki la Geita, limefungwa kuanzia jana Jumatatu hadi tarahe 18 Machi 2023, kwa ajili ya kusubiri utakaso wake baada ya kunajisiwa na mtu asiyejulikana. Anaripoti Mwandishi Wetu, Geita … (endelea).

Dikrii ya kufungwa kwa muda kanisa hilo imetolewa jana Jumatatu, tarehe 27 Februari 2023 na Askofu Jimbo Katoliki Geita, Flavian Kassala, ikiwa ni siku moja tangu mtu mmoja kuvamia na kufanya kufuru kwa kunajisi vifaa mbalimbslu vya ibada takatifu.

“Tukio hili ni uharufu mkubea sana ambao umeiathiri kwa kiasi kikubwa hadhi na muumini mkayoliki na jamii yetu kwa ujumla. Kutokana na matukio hayo kanisa hili limepoteza kwa kiasi kiku wa baraka yake kwa jamii,” imesema taarifa ya Askofu Kassala.

Taarifa hiyo imesema “waaminj wameumizwa sana kutokana na kashfa, kufuru na unajisi uliofanyika kwa imani yetu na hivyo naagiza kanisa hili halistahili kwa maadhimisho ya sakramenti ya ekaristi wala kwa ibada yoyote.”
Taarifa ya Askofu Kassala imesema kuwa, kanisa hilo litafunguliwa tarehe 18 Machi 2023, kwa adhimisho la ibada ya misa takatifu, itakayohusisha maadhimisho ya toba, malipizi na baraka.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Gardner Habash wa Clouds Fm afariki dunia

Spread the loveALIYEKUWA mtangazaji wa kipindi cha Jahazi kinachorushwa na kituo cha...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wauguzi, madaktari 1000 kugawiwa mitungi ya Oryx Gas

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gas na Taasisi ya Doris Mollel Foundation...

Habari Mchanganyiko

Tanzania yachaguliwa Makamu wa Rais Tume ya Shirika la Hali ya Hewa Duniani

Spread the love  TANZANIA kupitia Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)...

Habari Mchanganyiko

NEMC yaonya wanaojenga bila tathmini ya mazingira

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC),...

error: Content is protected !!