Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Michezo Kane aomba kuondoka Tottenham
Michezo

Kane aomba kuondoka Tottenham

Harry Kane
Spread the love

 

HARRY Kane, mshambuliaji Tottenham Hotspur ameandika barua ya kutaka kuondoka kwenye klabu hiyo licha ya kubakia na mkataba wa miaka mitatu na kuhusishwa kujiunga na klabu za Manchester City, Chelsea na Manchester United. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Kane mwenye umri wa miaka 27, anataka kuondoka kwenye klabu hiyo, ambayo alihudumu kwa kipindi cha miaka 12, licha ya kutowasilisha taarifa rasmi ya kwa maandishi.

Taarifa hizo zinakuja siku chache toka mchezaji huyo kunukuliwa kuwa “kwa sasa nahitaji timu ambayo nitashinda nayo mataji.”

Manchester City wanaongoza mbio za kumuwania mshambuliaji huyo, licha ya wamiliki wa klabu yake ya sasa kupambana kumbakisha kwenye viunga hivyo kwa kumuongezea mshahara.

Licha ya Manchester City kuingia kwenye kinyang’anyiro cha kutafuta saini ya mshabuliaji huyo, mabosi wa Manchester United walijitanabaisha wazi ya kuwa wapo tayari kutoa kiasi cha Euro 90 milioni (sawa Sh. 250.8 bilioni) kumnasa mshambuliaji huyo.

Ndani ya Ligi Kuu England, Kane amecheza jumla ya michezo 33, nakupachika kambani mabao 22, huku akitoa pasi za mwisho (assist) 13 na kutengeneza nafasi 47.

Kane pia katika michezo hiyo amepiga jumla ya mashuti 51 yaliyolenga goli na kupiga pasi 870.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Makala & UchambuziMichezo

TFF kuamua hatima ya Amrouche

Spread the loveHATIMA ya Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Adel Amrouche kuendelea...

Habari za SiasaMichezo

Matinyi: Dk. Ndumbaro alifanya utani ukaguzi mechi za Yanga, Simba

Spread the loveMsemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi amesema kauli iliyotolewa na...

Michezo

Gethsemane Group Kinondoni (GGK) waachia video ya Bwana Wastahili

Spread the loveWAIMBAJI maarufu nchini kutoka Gethsemane Group Kinondoni (GGK)SDA wameachia video...

BiasharaMichezo

Gamondi kocha bora mwezi Februari, NBC yamjaza manoti

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambae ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!