
Mwili wa aliyekuwa Mhariri wa MwanaHALISI Online, Edson Kamukara
MWILI wa aliyekuwa mhariri mwanzishi wa gazeti hili – MwanaHALISI Online – Edson Kamukara, umefikishwa salama kijijini kwao, Ihangiro, Muleba, mkoani Kagera. Anaripoti Desus Kahangwa, kutoka Muleba … (endelea).
Mwili wa Kamukara ulipofika uliingizwa ndani ya nyumba ya mama yake mzazi, kabla ya baadaye kupelekwa kwenye sehemu ya kuhifadhia maiti iliyopo kijijini hapo.
Kifo cha Kamukara, kilitokea juzi Alhamisi, nyumbani kwake majira ya saa 12: 30 jioni, Mabibo jijini Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa familia ya marehemu, shughuli za mazishi zitaanza kesho (Jumatatu), majira ya saa 5 asubuhi ambako misa ya kumuombea marehemu Kamukara itafanyika nyumbani kwa mama yake mzazi.
Mazishi yanatarajiwa kufanyika kati ya saa 9 jioni na saa 10.
More Stories
Huawei yaunga mkono malengo endelevu UN
Watuhumiwa 5 ujambazi wauawa Dar, bastola…
Takukuru yavimbia wakandarasi, ‘yarejesha’ mil 420 Tanesco