Friday , 29 September 2023
Home Kitengo Michezo Kampuni ya ndondi yaiburuza mahakamani Azam Media, yataka fidia Sh. 2 bil.
Michezo

Kampuni ya ndondi yaiburuza mahakamani Azam Media, yataka fidia Sh. 2 bil.

Spread the love

KAMPUNI inayojihusisha na uandaaji wa mapambano ya ngumi za kulipwa, Hall of Fame Boxing and Promotion, imeiburuza mahakamani Kampuni ya Azam Media, ikitaka ilipwe fidia ya Sh. mbili bilioni kwa madai imerusha maudhui yake katika runinga kinyume na makubaliano. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).

Kampuni hiyo imefungua kesi ya madai Na. 100/2023 katika Mahakama Kuu, Masjala Kuu ya Dar es Salaam, ikidai Azam Media ilikiuka makubaliano ya kimkataba kwa kurusha maudhui kwenye kipindi, yaliyohusu mapambano mawili.

Mkurugenzi wa Kampuni ya Hall of Fame Boxing and Promotion, Jay Msangi.

Mapambano hayo ni kati ya bondia Hassan Mwakinyo na rais wa Ufilipino, Arnel Tinampay na la Twaha Kiduku dhidi ya Dulla Mbabe, ambapo Azam Media inadaiwa kuyarusha bila ya kuwa na haki miliki ya maudhui hayo.

Inadaiwa kuwa makubaliano ya kimkataba  yaliyokuwepo baina ya wadai hao na Azam Media ni kurusha mapambano hayo mubashara (live) tu, lakini iliendelea kurusha marudio mapambano hayo kwa nyakati tofauti, kinyume na makubaliano.

Kampuni hiyo inadai kurudiwa kwa maudhui hayo kuliendelea kuinufaisha  Azam Media jambo ambalo linawasukuma kudai fidia hiyo. Pia, inadai Azam Media imerusha mapambano hayo bila kuweka nembo “logo” yake.

Kwa mujibu wa taarifa ya kampuni hiyo ya ndondi, imefikia uamuzi wa kufungua kesi baada ya jitihada za kutafuta suluhu katika mamlaka mbalimbali ikiwemo Taasisi ya Haki Miliki Tanzania (COSOTA), kutozaa matunda.

Kesi hiyo ya madai inatarajiwa kuanza kusikilizwa mahakamani hapo tarehe 18 Septemba 2023, mbele ya Jaji Mussa Pomo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Meridianbet yaibukia Tandika, yafungua duka jipya

Spread the love BAADA ya kupita maeneo mbalimbali hatimae kampuni yaMeridianbet imeibukia...

BiasharaMichezo

Ukiwa na Meridianbet ni rahisi kuwa milionea

Spread the love  CARABAO Cup raundi ya 3 Uingereza inaendelea na mechi...

Michezo

Jezi ya Samatta iliyoifunga Liverpool kuuzwa Genk

Spread the love  KLABU ya KRC Genk ya nchini Ubelgiji imeamua kuanza...

BiasharaMichezo

Hii ndio historia ya El-Clasico, derby bora zaidi duniani

Spread the love  KILA nchi ina vilabu viwili hasimu na pinzani nje...

error: Content is protected !!