Thursday , 25 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Kampuni kubwa nchini zashuka mtaji DSE
Habari Mchanganyiko

Kampuni kubwa nchini zashuka mtaji DSE

Ofisa Masoko wa DSE, Merry Kinabo
Spread the love

HALI ngumu ya kiuchumi imesababisha ukubwa wa mtaji wa kampuni kubwa zilizoorodheshwa katika Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE), kushuka kutoka Sh. trilioni 20.8 hadi kufikia SH. trilioni 20.4, anaandika Angel Willium.

Akizungumza na waandishi jijini Dar es Salaam, Ofisa Masoko wa DSE, Merry Kinabo ameyasema hayo leo.

Alitaja kampuni hizo kuwa ni pamoja na kampuni ya simu za mkononi ya Vodacom, Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) na Benki ya CRDB.

Ametaja sababu iliyochangia ukubwa wa mtaji wa kampuni hizo kushuka ni pamoja na kushuka kwa bei za hisa za KCB kwa asilimia 14, East Afrika Breweris Ltd (EABL) kwa asilimia 0.73 na National Media Group ( NMG) kwa asilimia 0.42.

Kinabo amesema kampuni zilizoorodheshwa katika Soko la Hisa (DSEI), zimeshuka kwa point 38 yaani kutoka 2,162 hadi 2,124 kutokana na kushuka kwa bei za kampuni ya KCB.

“Yaliyojiri kwenye soko la hisa kwa wiki iliyoishia Ijumaa iliyopita Oktoba 13, mwaka huu ukubwa wa mtaji wa makapuni ya VODA, TBL na CRDB umeshuka kimtaji pamoja na soko la DSEI zimeshuka kwa point 38 kutoka 2,162 hadi 2,124,’’ amesema

Aidha, thamani ya mauzo ya hisa imepanda kutoka Sh. Bilioni 1.5 ya wiki iliyoisha tarehe 13 0ktoba 2017 hadi Sh. Bilioni 30 na idadi ya hisa zilizouzwa na kununuliwa imepanda kutoka hisa laki 6 kwa wiki iliyoisha Oktoba 13 2017 hadi hisa milioni 2.5 .

Kampuni zilizoongoza kwa mauzo ya hisa ni kampuni ya VODA ,CRDB na TBL huku kampuni ya TSI ikipanda kwa point 11 kutoka point 3,814 hadi pointi 3,825 na kiashiria cha sekta ya viwanda (IA) kimepanda kutoka point 5,161 hadi 5,187.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

THRDC yaongeza mkataba wa ushirikiano na ABA

Spread the love  MTANDAO wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC),...

Habari Mchanganyiko

Rufaa ya Equity Benki, State Oil yakwama

Spread the loveMAHAKAMA ya Rufani, jijini Dar es Salaam, imeshindwa kuendelea na...

Habari Mchanganyiko

Bodaboda waeleza mafanikio mafunzo usalama barabarani

Spread the loveMADEREVA bodaboda katika Jiji la Dodoma wameeleza jinsi mafunzo ya...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC yaahidi kuendelea kuunga mkono Serikali za Mitaa

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imesisitiza dhamira yake ya...

error: Content is protected !!