Tuesday , 23 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Kambi ya Maalim Seif yatikiswa
Habari za Siasa

Kambi ya Maalim Seif yatikiswa

Spread the love

KAMBI ya Maalim Seif Shariff Hamad, Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF) imeendelea kutikiswa na utawala wa Rais John Magufuli baada ya mfuasi wake ambaye ni Mbunge wa Kilwa, Seleman Bungara ‘Bwege’ kukamatwa na kisha kutolewa kwa dhamana jana. Anaandika Faki Sosi … (endelea).

Bwege ambaye amejitenga na kambi ya Prof. Ibrahim Lipumba, Mwenyekiti wa CUF Taifa, alikumbana na dhahama ya kukamatwa na polisi jana kwa madai ya kutaka kufanya mkutoa bila kibali.

“Alikamatwa jana lakini hakulala, alitoka jana ile ile kwa kuwa, kilichokuwa kikitakiwa ni kukamilishi masharti ya dhamana na yalikamiika hivyo alitoka,” ameeleza Mbarara Maharagande, Mkurugenzi Habari na Mawasiliano CUF.

Bwege alikamatwa tarehe 1 Oktoba 2018 kwa tuhuma ya kutoaka kufanya mkutano bila kibali kwenye eneo linalotambulika kwa jina la Maalim Seif lililopo Kilwa Kivinje.

Taarifa zaidi zinaeleza kuwa, Bwege alitekeleza matakwa ya kisheria katika kupeleka barua kuwahabarisha polisi kuhusu mkutano wake, hata hiyo aliambiwa asifanye mkutano huo kwa maelezo kuwa hali ya usalama haipo imara.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Serikali kuanzisha mradi wa Gridi ya maji ya Taifa

Spread the loveWaziri wa Maji, Jumaa Aweso amesema katika mwaka wa fedha...

Habari za Siasa

Rais Samia aridhishwa utendaji mabalozi, awapa neno

Spread the loveRais wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan amewapongeza mabalozi  wanaowakilisha ...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

NMB yadhamini Mkutano Mkuu ALAT, kufunguliwa na Samia

Spread the loveBENKI ya NMB, imekabidhi hundi yenye thamani ya Sh. 120...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mipango na uwekezaji kutumia bilioni 121.3, mradi wa Bagamoyo wapewa kipaumbele

Spread the loveWIZARA ya Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, imeliomba Bunge...

error: Content is protected !!