Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Kambi Rasmi ya upinzani Bungeni, njiapanda
Habari za SiasaTangulizi

Kambi Rasmi ya upinzani Bungeni, njiapanda

Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa Chadema
Spread the love

KAMBI Rasmi ya upinzani bungeni, iko hatarini “kusambaratika” kufuatia “mapinduzi” ya kisiasa, yaliyotokea ndani ya Chama cha Wananchi (CUF). Anaripoti Danson Kaijage kutoka Dodoma … (endelea).

Taarifa zilizopatikana kutoka kwa baadhi ya wabunge wa CUF zinasema, ni vigumu mno kwa wabunge wa chama hicho, kuendelea kushirikiana na wenzao wa Chadema, katika uendeshaji wa kambi hiyo.

Kambi rasmi ya upinzani bungeni, ilikuwa inaundwa na wabunge kutoka vyama vya NCCR- Mageuzi, chama cha ACT- Wazalendo, Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) na baadhi ya wabunge kutoka CUF.

Uwezekano wa “kusambaratika” kwa kambi hiyo, unatokana na hatua ya mwenyekiti wa CUF, Prof. Ibrahim Lipumba, kutangaza kutoshirikiana na vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA).

Kambi Rasmi ya upinzani bungeni, inaongozwa na Freeman Mbowe, mbunge wa Hai (Chadema) na mwenyekiti wa taifa wa chama hicho.

Hata hivyo, mwenyekiti wa Kamati ya Uongozi ya wabunge wa CUF, Suleman Bungara (Bwege), ameeleza MwanaHALISI Online kuwa yeye na baadhi ya wenzake, hawaamini katika utengano.

Anasema, “mimi naamini katika umoja. Siamini katika utengano. Nje ya umoja, hatuwezi kushinda jimbo lolote la uchaguzi. Hata pale Kilwa, hatuwezi kushinda kama hatutakuwa na umoja.”

Akizungumzia kauli ya Prof. Lipumba, mbunge huyo wa Kilwa Kusini anasema, “huyo amesema yeye kama yeye na siyo kama taasisi.”

Anaongeza, “…kauli yake haijatokana na vikao vya Baraza Kuu ama Kamati Kuu (Kamati Tendaji), ni kauli yake binafsi. Na mimi naichukulia hivyo. Na kwa msingi huo, mimi binafsi nitaendelea kushirikiana na UKAWA.”

“Kushinda bila kushirikiana hakuwezekani, kama tunataka ushindi ni lazima tushirikiane. Kama Prof. Lipumba alisema hayo, pengine ni kutokana na mgogoro uliyokuwapo. Sisi tutaendeelaa kushirikiana kwa msingi kwamba umoja ni nguvu na utengano ni udhaifu.”

Chama cha CUF, kimekubwa na mgawanyiko mkubwa uliokimega chama hicho mapande mawili, kufuatia Prof. Ibrahim Lipumba, kurejeshwa kwenye uongozi wa chama hicho na Msajili wa Vyama vya Siasa, Jaji Francis Mutungi.

Kufuatia maamuzi hayo, aliyekuwa katibu mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad, pamoja na wafuasi wake waliamua kwenda mahakamani na baadaye wakatangaza kukihama chama hicho na kujiunga na ACT- Wazalendo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

Habari za Siasa

Wabunge waikalia kooni TAKUKURU Bungeni

Spread the love  BAADHI ya wabunge wamelia na changamoto za utendaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

error: Content is protected !!