Tuesday , 23 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Kamati ya Bunge yashauri TIC iwe mamlaka kamili
Habari za Siasa

Kamati ya Bunge yashauri TIC iwe mamlaka kamili

Waziri Mkuu akihutubia Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Spread the love

 

KAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira, imependekeza kuwa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) kipewe mamlaka kamili badala ya kuwa wakala wa Serikali. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Akisoma maoni ya kamati kuhusu Muswada wa Sheria ya Uwekezaji Tanzania ya mwaka 2022, leo Jumanne tarehe 1 Novemba, 2022, bungeni jijini Dodoma, Mwenyekiti wa Kamati hiyo, David Kihenzile amesema hadhi ya TIC haiwezeshi mfumo Madhubuti wa kitaasisi kwaajili ya uratibu na uwezeshaji wa uwekezaji nchini.

“Kwa sababu hiyo, Kamati inapendekeza Kituo cha uwekezaji kipewe Mamlaka kamili badala ya kuendelea kuwa Wakala wa Serikali, lengo ni kukipa nguvu ya utekelezaji wa majukumu yake,” amesema Kihenzile.

Kamati inapendekeza pia kuwa baada ya Sheria hiyo kutungwa na Bunge ‘‘itafsiriwe katika Lugha ya Kiingereza ndani ya siku 30.

Sababu ni uhalisia wa Uwekezaji ambao kutokana na vivutio katika Muswada huu Wawekezaji wengi wanatarajiwa kutoka mataifa mbalimbali.”

Pia kamati imetoa maoni na mapendekezo ya mabadiliko ya baadhi ya vifungu ikiwemo Kifungu cha kwanza kuhusu Jina la sheria hiyo.

“Kamati inashauri Jina la Sheria lisomeke Sheria ya kuvutia na kulinda Uwekezaji Tanzania ya mwaka 2022,” amesema.

Aidha katika Kifungu cha 3 cha Tafasiri, Kamati imeshauri kuongezeke Maneno ‘ardhi’ na ‘Hakimiliki’ kwenye tafsiri ya neno ‘Mtaji’.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Rais Samia aridhishwa utendaji mabalozi, awapa neno

Spread the loveRais wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan amewapongeza mabalozi  wanaowakilisha ...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

NMB yadhamini Mkutano Mkuu ALAT, kufunguliwa na Samia

Spread the loveBENKI ya NMB, imekabidhi hundi yenye thamani ya Sh. 120...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mipango na uwekezaji kutumia bilioni 121.3, mradi wa Bagamoyo wapewa kipaumbele

Spread the loveWIZARA ya Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, imeliomba Bunge...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mbunge ataka kasi uzalishaji walimu ipunguzwe akidai hakuna ajira

Spread the loveMBUNGE wa Mlalo (CCM), Rashid Shangazi, ameishauri Serikali ipunguze kasi...

error: Content is protected !!