Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Kamati ya Bunge yaitaka Serikali ichukue hatua kudhibiti mfumuko wa bei
Habari za Siasa

Kamati ya Bunge yaitaka Serikali ichukue hatua kudhibiti mfumuko wa bei

Waziri Mkuu akihutubia Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Spread the love

 

SERIKALI ya Tanzania imetakiwa kufanya tathimini dhidi ya changamoto ya kupanda kwa bei ya mahitaji muhimu ikiwemo vyakula, ili iweze kuchukua hatua za haraka kuidhibiti. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Wito huo umetolewa leo Jumatano, tarehe 1 Februari 2023 na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira, wakati ikiwasilisha bungeni taarifa yake ya shughuli ilizotekeleza kuanzia Februari 2022 hadi Februari 2023.

Akiwasilisha taarifa hiyo, Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira, David Kihenzile, amesema Serikali inatakiwa kuweka mikakati ya muda mrefu ili kuzuia hali hiyo.

“Kutokana na changamoto ya kupanda kwa bei ya mahitaji muhimu ikiwemo Mafuta, Mchele na Sukari, ni Rai ya Kamati kwamba Serikali itathimini hali hiyo na ichukue hatua za haraka sambamba na kuweka mikakati ya muda mrefu ili kuzuia hali hiyo,” amesema Kihenzile akisoma taarifa hiyo.

Wito wa kamati hiyo imekuja ikiwa imepita siku moja tangu baadhi ya wabunge kuitaka Serikali kuchukua hatua madhubuti kudhibiti changamoto ya mfumuko wa bei za vyakula, ili kuwasaidia wananchi masikini ambao hawana kipato cha kutosha kumudu mfumuko huo.

Hata hivyo, Serikali imetoa taarifa bungeni ya kwamba jitihada ilizochukua katika kutoa ruzuku kwenye mafuta, mbolea na maeneo mengine, itasaidia kuondoa mfumuko huo katika msimu ujao wa mavuno.

Kwa kuwa katika msimu wa 2022/23, wakulima wamefanya shughuli za uzalishaji kwa gharama nafuu baada ya Serikali kuweka ruzuku.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Chadema yamtaka Rais Samia aunde tume kuchunguza mauaji mgodi wa Barick

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, ameombwa aunde tume huru kwa...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

error: Content is protected !!