KAMATI Kuu ya Halmashauri Kuu ya chama tawala nchini Tanzania- Chama Cha Mapinduzi (CCM) leo Jumanne, tarehe 21 Juni 2022 inakutana jijini Dodoma. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).
Ukurasa wa kijamii wa Twitter wa CCM umesema, kikao hicho kitafanyikia jijini Dodoma na kuongozwa na mwenyekiti wake ambaye pia ni Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan.
Agenda za kikao hicho hazijajulikana lakini chama hicho tawala kinakutana kipindi ambacho kuna fukuto ndani ya nchi mbili wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki ambazo ni Burundi na Rwanda.
Huenda chama hicho tawala kikazungumzia suala hilo na kulitolea taarifa ama kulijadili suala hilo.
Leave a comment