Thursday , 30 March 2023
Home Gazeti Habari Mchanganyiko Kajala, Paulina wahojiwa polisi
Habari Mchanganyiko

Kajala, Paulina wahojiwa polisi

Spread the love

 

JESHI la Polisi Tanzania, limeeleza kwamba lilimkamata mwigizaji Kajala na mwanaye Paulina kwa tuhuma za kusambaza picha za utupu za msanii wa Bongo Fleva, Rajab Abdul ‘Harmonize.Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam.

Lazaro Mambosasa, Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam amesema, wawili hao walikamatwa jana muda mfupi baada ya kutua katika ardhi ya Tanzania wakitokea Dubai.

Hata hivyo amesema, baada ya mahojiano na wawili hao, waliachwa kwa dhamana.

SACP Lazaro Mambosasa, Kamanda wa Jeshi la Polsii Kanda Maalumu ya Dar es Salaam

“Tuliwakamata na tukawahoji baada ya mlalamikaji (Harmonize) kuleta malalamiko kituoni, hata hivyo tayari tumewaachia kwa dhamana,” amesema Kamanda Mambosasa.

Pamoja na kuachwa kwa dhamana, Kamanda Mambosasa amesema, wawili hao wataendelea kuripoti kituo cha polisi mpaka pale uchunguzi utakapokamilika na kisha kupelekwa mahamani.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

NMB Bonge la Mpango – ‘Moto Uleule’ yazinduliwa, Milioni 180…

Spread the loveMSIMU wa tatu wa Kampeni ya kuhamasisha utamaduni wa Kuweka...

Habari Mchanganyiko

Rais Samia awataka wahariri kufanya kazi bila uoga, upendeleo

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan amewataka wahariri wa vyombo...

Habari Mchanganyiko

STAMICO yasaini mkataba wa bilioni 55.2 kuchoronga miamba GGML

Spread the loveSHIRIKA la Madini la Taifa (STAMICO) limezidi kufanya vizuri katika...

Habari Mchanganyiko

NMB yatoa traksuti za Mwenge wa Uhuru Mtwara

Spread the loveBENKI ya NMB imetoa traksuti kwa mkoa wa Mtwara ambako...

error: Content is protected !!