Friday , 29 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Kajala, Paulina wahojiwa polisi
Habari Mchanganyiko

Kajala, Paulina wahojiwa polisi

Spread the love

 

JESHI la Polisi Tanzania, limeeleza kwamba lilimkamata mwigizaji Kajala na mwanaye Paulina kwa tuhuma za kusambaza picha za utupu za msanii wa Bongo Fleva, Rajab Abdul ‘Harmonize.Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam.

Lazaro Mambosasa, Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam amesema, wawili hao walikamatwa jana muda mfupi baada ya kutua katika ardhi ya Tanzania wakitokea Dubai.

Hata hivyo amesema, baada ya mahojiano na wawili hao, waliachwa kwa dhamana.

SACP Lazaro Mambosasa, Kamanda wa Jeshi la Polsii Kanda Maalumu ya Dar es Salaam

“Tuliwakamata na tukawahoji baada ya mlalamikaji (Harmonize) kuleta malalamiko kituoni, hata hivyo tayari tumewaachia kwa dhamana,” amesema Kamanda Mambosasa.

Pamoja na kuachwa kwa dhamana, Kamanda Mambosasa amesema, wawili hao wataendelea kuripoti kituo cha polisi mpaka pale uchunguzi utakapokamilika na kisha kupelekwa mahamani.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Puma Energy Tz: Watanzania tudumishe amani kuvutia uwekezaji

Spread the loveKAMPUNI ya Mafuta ya Puma Tanzania imewakutanisha wadau mbalimbali katika...

Habari Mchanganyiko

DAWASA waanza utekelezaji agizo la Samia

Spread the loveMamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam...

Habari MchanganyikoKimataifa

Zuma akataliwa kugombea urais

Spread the loveTUME Huru ya Uchaguzi Afrika Kusini (IEC) imemwondoa rais wa...

Habari Mchanganyiko

Mtandao watetezi wa haki za mazingira Tanzania waundwa

Spread the loveMTANDAO wa watetezi wa haki za mazingira nchini Tanzania, umeundwa...

error: Content is protected !!