Thursday , 28 March 2024
Home Habari Mchanganyiko JWTZ watangaza kiama kwa matapeli ajira jeshini
Habari Mchanganyiko

JWTZ watangaza kiama kwa matapeli ajira jeshini

Spread the love

Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), limetoa ufafanuzi kuhusu vitendo vya rushwa, ulaghai na utapeli vinavyofanywa na baadhi ya watu wasio waaminifu, wakiwaahidi watu mbalimbali kwamba watawasaidia kupata nafasi ya kuandikishwa katika nafasi za ajira zilizotangazwa na jeshi hilo. Anaripoti Rhoda Kanuti… (endelea).

Akizungumza na waandishi wa habari leo tarehe 30 Novemba, 2021 jijini Dar es Salaam, Kaimu Mkurugenzi wa Habari na Uhusiano wa JWTZ, Luteni Kanali Gaudentius Ilonda amesema matapeli hao wameenda mbali zaidi na kutumia jina la mkuu wa majeshi.

Amesema matapeli hao wanadai kuwa Mkuu huyo wa majeshi ndiye aliyewatuma kukusanya fedha ili wapate nafasi ya kuandikishwa, jambo ambalo si la kweli.

Aidha, amewataka wananchi kutoa taarifa haraka endapo watakutana na watu wa aina hiyo, na kusisitiza kwamba jeshi halina utaratibu wa kuwatoza watu fedha ili wapate nafasi ya kujiandikisha na kwamba wanaofanya vitendo hivyo ni matapeli.

Aidha, amewaonya baadhi ya wazazi ambao wameanza kuwatafuta viongozi serikali na kuwaomba vijana wao wajiunge na jeshi hilo kwa visingizio mbalimbali.

“Jeshi haliandikishi vijana kwa kutafuta pesa bali ni jeshi ambalo linafuata sheria na sifa kwa  kijana.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Soko nepi za watoto lashuka, watu wazima lapaa

Spread the loveKiwanda cha kutengeneza nepi cha Japan kimetangaza kuwa kitaacha kutengeneza...

error: Content is protected !!