Thursday , 25 April 2024
Home Kitengo Michezo JWTZ kushiriki mashindano ya majeshi duniani
Michezo

JWTZ kushiriki mashindano ya majeshi duniani

Kanali Joseph Bakari, Mwakilishi wa Baraza la Michezo la Majeshi Duniani (CISM)
Spread the love

JESHI la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), linatarajia kushiriki michezo ya majeshi ya dunia itakayofanyika nchini China kuanzia tarehe 18 hadi 27 Oktoba mwaka huu. Anaripoti Regina Mkonde…(endelea).

Kauli hiyo imetolewa na Kanali Joseph Bakari, Mwakilishi wa Baraza la Michezo la Majeshi Duniani (CISM), wakati akizungumza na wanahabari leo tarehe 3 Julai 2019, jijini Dar es Salaam.

Akizungumzia kuhusu maandalizi ya michuano hiyo Kanali Bakari amesema, JWTZ imeandaa mikakati thabiti itakayowezesha timu zake zitakazoshiriki zinashinda.

Kanali Bakari amesema, JWTZ itashiriki michezo 3 kati ya 27 ikiwemo mchezo wa masumbwi, mieleka na riadha.

“Tanzania tulikuwa tunafanya vizuri katika michezo miwili, boxing na riadha kwa wakati huo. Tunatarajia kushiriki katika michezo mitatu ambayo ni ngumi, mieleka na riadha.

“Mìkakati inafanyika, ukiangalia takwimu ni kweli tulikuwa hatufanyi vizuri, tunalichukua na kuweka mkakati na sisi tufanye vizuri,” amesema Kanali Bakari.

Amesema, dhumuni la michuano hiyo ni kutumia michezo kama njia ya kueneza amani duniani badala ya vita.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

EPL, Ligue 1 na Coppa Italia kinawaka leo

Spread the love  LEO ligi kadhaa zitaendelea nchini barani ulaya ikiwemo ligi...

BiasharaMichezo

NBC yaunga mkono jitihada kutokomeza malaria

Spread the loveKuelekea Maadhimisho ya siku ya malaria Duniani yatakayofanyika kesho Aprili...

Michezo

Arsenal dhidi ya Chelsea ngoma nzito leo EPL

Spread the love  Leo kutakua na mchezo mkali sana pale kwenye ligi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC yanogesha Derby Kariakoo, Aziz Ki aibuka mchezaji bora Machi

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambayo ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!