Thursday , 25 April 2024
Home Kitengo Michezo Julio alia na wachezaji Stars, ataka wajiongeze
Michezo

Julio alia na wachezaji Stars, ataka wajiongeze

Jamhuri Kihwelu 'Julio'
Spread the love

 

KOCHA wa timu ya Taifa ya Vijana chini ya miaka 20 (NgorongoroHeroes), Jamhuri Julio amelia na namna ya wachezaji wa timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ kuwa walishindwa kujiongeza mpaka kuondolewa kwenye michuano ya Kombe la Mataifa Afrika kwa wachezaji wa ndani (CHAN) baada ya kutoka sare ya mabao  2-2 na Guinea. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Taifa stars iliondolewa kwenye michuano hiyo inayoendelea nchini Cameroon baada ya kumaliza kwenye nafasi ya tatu kundi D, wakiwa na pointi nne.

Akiongea mbele ya waandishi wa habari leo tarehe 1 Februari 2021, kocha huyo alisema kuwa wakati Stars inaongoza 2-1 dhidi ya Guinea wachezaji walipaswa kujiongeza na siyo kila kitu kumuachia kocha ili waweze kuibuka na ushindi.

“Tunaweza kuwaona makocha wabovu au hawafai, mwalimu anafundisha mbinu na ufundi kuna muda wachezaji wanatakiwa wabuni wenyewe kwa kujiongeza ili waweze kushinda lakini siyo kila kitu mwalimu apige kelele,” alisema Julio.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

EPL, Ligue 1 na Coppa Italia kinawaka leo

Spread the love  LEO ligi kadhaa zitaendelea nchini barani ulaya ikiwemo ligi...

Michezo

Arsenal dhidi ya Chelsea ngoma nzito leo EPL

Spread the love  Leo kutakua na mchezo mkali sana pale kwenye ligi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC yanogesha Derby Kariakoo, Aziz Ki aibuka mchezaji bora Machi

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambayo ni mdhamini Mkuu...

Michezo

Ujanja ni kubeti na Meridianbet

Spread the love  JUMAPILI ya leo imekaa kihela hela sana ndani ya...

error: Content is protected !!