Friday , 29 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Jukwaa la kuwawezesha wanawake kiuchumi lazinduliwa
Habari Mchanganyiko

Jukwaa la kuwawezesha wanawake kiuchumi lazinduliwa

Spread the love

 

JUKWAA la kitaifa la kuwawezesha wanawake kiuchumi limezinduliwa ili kuliwezesha kundi hilo kufikia fursa zinazowazunguka. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Uzinduzi huo umefanywa hivi karibuni jijini Dodoma na Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, kwa kushirikiana na Taasisi ya Legal Services Facility.

Akizungumza wakati wa ufunguzi huo, Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Dk. Dorothy Gwajima, amesema jukwaa hilo limeanzishwa ili kuongeza uelewa kwa wanawake kuhusu masuala ya Biashara, upatikanaji mitaji na Sheria za nchi katika masuala ya uchumi.

Amesema mbali na jukwaa hilo la kitaifa, Serikali imeunda majukwaa ngazi ya mkoa katika mikoa 26 ya Tanzania Bara.

Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Dk. Dorothy Gwajima

“Kupitia maazimio ya mkutano wa wanawake Beijing 1995, Tanzania iliamua kujikita katika maeneo manne ambayo ni: kuwawezesha wanawake kiuchumi; wanawake na haki za kisheria; usawa katika elimu, mafunzo na ajira; na wanawake katika nafasi za uongozi na ngazi za Maamuzi.”

Waziri huyo wa maendeleo ya Jamii amesema “pia, mwaka 2021, Tanzania ilishiriki Mkutano wa Kimataifa wa Jukwaa la Kizazi chenye Usawa (Generation Equality Forum) uliofanyika Jijini Paris – Ufaransa, ambapo Tanzania iliwasilisha ahadi za nchi, ambazo Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, ni kinara katika utekelezaji wa eneo linalohusu haki na Usawa wa Kiuchumi.”

Katika hatua nyingine, Dk. Gwajima ameyaagiza majukwaa hayo nchi nzima kuwaunganisha wanawake katika fursa za kibenki, masoko na utaalamu wa kuboresha uzalishaji wa bidhaa zao.

Mkurugenzi Mtendaji wa Legal Services Facility (LSF), Lulu Ng’wanakilala

Mkurugenzi Mtendaji wa Legal Services Facility (LSF), Lulu Ng’wanakilala, amesema Shirika hilo imeamua kushirikiana na Serikali katika uzinduzi wa jukwaa hilo, kwa kuwa linagusa moja ya maeneo muhimu ya utekelezaji wa programu ya upatikanaji wa haki kwa watu wote.

“Ni matumaini yetu kuwa Jukwaa hili la kitaifa litajikita katika kusghulikia changamoto mbalimbali za wanawake kwenye masuala ya kiuchumi, masuala ya kisera, kitaaluma, kirasilimali pamoja na haki nyingine za msingi za kiuchumi. Sisi kama LSF tutaendelea kushirikiana na Jukwaa hili kupitia Wizara ya Maendeleo ya Jamii,” amesema Ng’wanakilala.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mtandao watetezi wa haki za mazingira Tanzania waundwa

Spread the loveMTANDAO wa watetezi wa haki za mazingira nchini Tanzania, umeundwa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

error: Content is protected !!