Thursday , 25 April 2024
Habari za Siasa

JPM: Hakuna vya bure

Aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania hayati Dkt John Magufuli
Spread the love

 

RAIS John Magufuli amewaambia wakazi wa Bahi, Dodoma na Tanzania kwa ujumla kwamba, ‘hakuna vya bure.’ Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Amesema, kila mtua anapaswa kufanya kazi na kwamba, katika utawala wake, anataka kila mtu afanye kazi kwani si kazi ya serikali kumlisha mtu.

“Ninawaomba watanzani zangu wa Bahi tuchape kazi, vya bure havipo,” amesema Rais Magufuli akiwa Bahi kuelekea Dodoma akitokea katika ziara mkoani Shinyanga leo tarehe 31 Januari 2021.

Akizungumzia kilimo cha mahindi na tabia ya uvivu kwa baadhi ya wakazi wa Bahi, amehoji inawezekanaje shambo moja likalimwa halafu lingine likawa na pori?

“Haiwezekani mwingine amewivisha mahindi yameweka mbelewele halafu shamba la mtu anayefuata naye hajalima chochote, kuna majani. Hiyo haikubaliki.

“Tunataka hii fedha tunayoitapa ikafanye miradi mkubwa. Tunajenga reli ya kisasa kutoka Dar es Salaam, Morogoro, Dodoma mpaka Maktupora. Tukimaliza tunataka tuiunganishe hii reli kutoka Maktupora, Tabora mpaka iende Mwanza na iende Kigoma, hiyo ndio kazi ya serikali,” amesema.

Na kwamba, serikali inajenga hospitali, inanunua ndege na inatengeneza barabara kwa sabaubu ndio kazi yake.

“Tunajenga hosptali hiyo ndio kazi ya seikali, tunanunua ndege hiyo ndio kazi ya serikali, tunatengeneza barabara hiyo ndio kazi ya serikali.

“Tunaleta madawa kwenye hospitali ndio maana bajeti tumeiongeza … lakini kukulisha ni kazi yako. Ninawaomba, vyabure havipo,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!