Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa JPM awaweka njia panda Dk. Kigangwalla, Prof. Mkenda
Habari za Siasa

JPM awaweka njia panda Dk. Kigangwalla, Prof. Mkenda

Spread the love

RAIS John Magufuli ametoa siku tano kwa Dk. Hamisi Kigwangalla, Waziri wa Maliasili na Utalii na Prof. Adolf Mkenda, Katibu Mkuu wa wizara hiyo, kuondoa tofauti zao vingenevyo ‘atawatumbua’. Anaripoti Regina Mkonde…(endelea).

Rais Magufuli ametoa agizo hilo leo tarehe 31 Desemba 2019, wakati akizungumza na Maafisa na Askari wa Wanyamapori wa Hifadhi ya Taifa ya Kisiwa cha Rubondo ….

Kiongozi huyo wa nchi amesema mahusiano mabaya ya  Dk. Kigwangalla na Prof. Mkenda yanasababisha baadhi ya shughuli za wizara hiyo, kukwama.

“Nnafahamu watendaji wenu wa juu Katibu Mkuu wa Wizara kila siku wanagombana, na ninawatazama taratibu. Nilishampa kazi Katibu Mkuu Kiongzi awaite, awaeleze lakini wasipobadilika nitawaondoa. Hilo ni lazima nizungumze kwa dhati,” ameagiza Rais Magufuli na kuongeza;

“Siwezi kuwa na watendaji wa kuteua mimi halafu kila siku wanagombana, kuna mambo mengi hayaendi. Katibu Mkuu hamheshimu Waziri n Waziri nae hataki kwenda na Katibu Mkuu, siwezi kuvumilia hilo.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!