RAIS John Magufuli amegoma kupokea wanachama wapya wanaotaka kujiunga na Chama Cha Mapinduzi (CCM). Anaandika Faki Sosi … (endelea).
Taarifa za awali zinadai kuwa, kulikuwa na watu waliotaka kujiunga na chama hicho mbele yake.
Akiwa katika ziara ya kikazi mjini Nansio, Ukerewe mkoani Mwanza leo Septemba 4, 2018 Rasi Magufuli alisema, ziara yake ni ya kikazi na sio ya kisiasa.
“Najua nikisema hapa wanaotaka kuhamia CCM wajitokeza watakuja wengi.
“Lakini sitaki kufanya hivyo kwa sababu ziara yangu na mkutano huu siyo wa kisiasa. Wafanye hivyo kwenye vikao rasmi,” amesema Rais Magufuli.
Leave a comment