Monday , 5 June 2023
Home Gazeti Habari za Siasa JPM: ATCL imekusanya Bil. 32.7
Habari za Siasa

JPM: ATCL imekusanya Bil. 32.7

Spread the love

RAIS John Magufuli amesema Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) limekusanya mapato, kiasi cha Dola 14 milioni (sawa na TSh. 32.7 bilioni). Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Rais Magufuli amesema hayo leo tarehe 26 Oktoba 2019, katika hafla ya upokeaji ndege mpya ya serikali aina ya Boeing 787-8 Dreamliner, iliyofanyika jijini Dar es Salaam.

Rais Magufuli amesema mapato hayo yametajwa na Mhandisi Isack Kamwelwe, Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, na kuwa,  atafuatilia mapato hayo kama ni kweli.

“Hizi zimenunuliwa kwa fedha za serikali hazijanunuliwa na ATCL, tumewaazima wazitumie kufanya biashara, na biashara lazima izalishe. Nilimuuliza waziri amesema wana Dola 14 miliono, nitakwenda kuzicheki kesho kwenye akaunti,” amesema Rais Magufuli.

Rais Magufuli ameuagiza uongozi wa ATCL kutekeleza majukumu yao vizuri, ili shirika hilo lijiendeshe kwa faida.

“Nitoe wito, kwanza kwa management (uongozi) na watumishi wa ATCL, tekelezeni majukumu yenu vizuri,” amesema Rais Magufuli.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Lusinde: CCM hatuliachii ng’o jimbo la Moshi Mjini

Spread the loveMJUMBE wa Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (NEC), Livingston...

Habari za SiasaTangulizi

Serikali ya Mapinduzi Zanzibar: Bakharesa hajavamia shamba letu

Spread the love  IKULU Visiwani Zanzibar, imeeleza kuwa eneo la kiwanda cha...

Habari za SiasaTangulizi

Zanzibar watangaza rasmi kuwa shamba la Razaba ni mali yao

Spread the love  SERIKALI ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), imetangaza rasmi kwamba shamba...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Mwinyi azindua Kamati ya Maridhiano Visiwani

Spread the love  RAIS wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), Dk. Hussein...

error: Content is protected !!