Tuesday , 5 December 2023
Habari za Siasa

JPM amtumbua mwingine

Rais John Magufuli
Spread the love

WAKILI Julius Kalolo, ameteuliwa na Rais John Magufuli kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Wakala wa Umeme Vijijini (REA). Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Taarifa ya uteuzi huo imetolewa jana tarehe 17 Juni 2019 na Mkurugenzi wa Mawasiliani ya Rais-Ikulu, Gerson Msigwa.

Taarifa ya Msigwa inaeleza kuwa, uteuzi wa Wakili Kalolo umeanza rasmi jana.

Aidha, taarifa hiyo imeeleza kwamba uteuzi wa Wakili Kalolo umefuatia hatua ya Rais Magufuli kutengua uteuzi wa aliyekuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya REA, Michael Nyagoga.

“Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli ametengua uteuzi wa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Bw. Michael Pius Nyagoga kuanzia leo (jana) tarehe 17 Juni, 2019,” imeeleza taarifa ya Msigwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Dk. Biteko: Viongozi tuache alama nzuri katika utendaji wetu

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

Habari za SiasaTangulizi

Chanzo maporomoko yaliyoua 65 Hanang, chatajwa

Spread the loveSERIKALI imesema kumeguka kwa sehemu ya Mlima Hanang ambao ilikuwa...

Habari za Siasa

Baba yake Ole Sabaya ashinda Uenyekiti CCM – Arusha

Spread the loveLoy Thomas Sabaya ambaye ni Baba wa aliyekuwa Mkuu wa...

Habari za Siasa

Serikali yaagiza uchunguzi chanzo maporomoko Hanang

Spread the loveSERIKALI imeagiza uchunguzi ufanyike ili kubaini chanzo cha maporomoko ya...

error: Content is protected !!