Tuesday , 30 May 2023
Home Gazeti Habari za Siasa JPM ampuuza mbunge CCM
Habari za SiasaTangulizi

JPM ampuuza mbunge CCM

Rais John Magufuli
Spread the love

RAIS John Magufuli amepuuza tuhuma zilizotolewa na Janeth Mbene, Mbunge wa Ileje kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) dhidi ya Haji Mnasi, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ileje mkoani Songwe, kwamba hana ushirikiano. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Licha ya Mbene kumchongea Haji kwa rais leo tarehe 5 Oktoba 2019, kiongozi huyo wa nchini amesema ‘simfukuzi’.

Mbunge huyo alimwambia Rais Magufuli, kwamba mteule wake (Haji) hana ushirikiano na watendaji wengine katika halmashauri hiyo, hivyo kusababisha utendaji kuwa mgumu.

Akizungumza na wananchi kwenye mji mdogo wa Mpemba, mkoani humo, Rais Magufuli amesema, hana taarifa za tuhuma anazohusishwa Haji ikiwemo wizi.

“Sasa mkurugenzi simtoi hadi nipate taarifa zangu mwenyewe,” amesema Rais Magufuli na kuongeza; “…sina uhakika kama dhambi zote hizo ni za mkurugenzi.

“Taarifa niliyonayo mimi na Jafo (Seleman-Waziri wa Tamisemi ni shahidi kwamba huyu mkurugenzi saa nyingine anaacha kazi zake za ofisini anaenda kufundisha darasani.”

Akizungumzia tuhuma za Haji, Rais Magufuli amesema hawezi kuchukua hatua yoyote jambo ambalo litakuwa uonevu.

“…mkurugenzi uko hapa, sikutoi mpaka nipate information (taarifa) zangu mwenyewe,” kauli hiyo ilipokelewa kwa tabasamu na mkurugenzi huyo.

Hata hivyo, kwenye mkutano huo alikuwepo Suleiman Jafo, Waziri wa Ofisi ya Rais-TAMISEMI ambapo rais alimuuliza kuhusu tuhuma anazobebeshwa Haji.

Jafo alimjibu Rais Magufuli kwamba katibu wa wizara hiyo yupo kwenye uchunguzi. Mdipo Rais Magufuli aliposema “mnaona, kumbe hata hiyo taarifa haijafika kwa Waziri wa Tamisemi, sasa mimi nichukue hatua tu yakufukuza mtu? ati jamani si nitawaonea watu kila mahali?.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Uamuzi juu ya wakurugenzi kusimamia uchaguzi 13 Juni

Spread the love  MAHAKAMA ya Afrika ya Haki za Binadamu (ACHPR), imepanga...

Habari MchanganyikoTangulizi

Jeshi la Polisi kushirikiana na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam katika utafiti

Spread the love  JESHI la Polisi Nchini limesema kuwa katika kukabiliana na...

KimataifaTangulizi

Mtuhumiwa wa mauaji ya halaiki ya Rwanda akamatwa Afrika Kusini

Spread the love  MMOJA wa watuhumiwa wakuu wa mauaji ya Kimbari ya...

Habari za Siasa

Musoma Vijijini waomba ujenzi wa barabara uanze haraka

Spread the loveJIMBO la Musoma Vijijini, mkoani Mara, limeomba Serikali kuhakikisha ujenzi...

error: Content is protected !!