Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa JPM amaliza utata wa JKT, Uyole na wananchi
Habari za Siasa

JPM amaliza utata wa JKT, Uyole na wananchi

Rais John Magufuli
Spread the love

RAIS John Magufuli amemaliza mvutano wa ardhi uliokuwepo kati ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), wananchi na Kituo cha Utafiti wa Kilimo (Uyole) wilayani Nkasi, Rukwa. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

 Leo tarehe 8 Oktoba 2019, Rais Magufuli ameamua, katika ekari 27,000 zilizokuwa mikononi mwa JKT, Uyole wabaki na ekari 4,000 na ekari 1,000 ziende kwa wananchi.

Umuzi huo umetokana na malalamiko ya wananchi wa Kijiji cha Kalongwe kupitia diwani wao, kwamba hawana maeneo kwa ajili ya kilimo.

Kwenye ziara ya Rais Magufuli wilayani Nkasi, mkuu wa kikosi cha JKT wilayani humo amemweleza rais kwamba, awali kikosi hicho kilikuwa kikimiliki ekari 27,000 na baadaye kiliipa Uyole ekari 5,000.

“Siwezi kupunguza eneo la jeshi” amesema Rais Magufuli na kueleza kuwa, Uyole sasa wabaki na ekari 4,000 huku ekari 1,000 ziende kwa wananchi kwa ajili ya kilimo.

Hata hivyo, Rais Magufuli amewapongeza JKT kwa kazi zao wanazozifanya na kwamba wanafanya vizuri kwenye maeneo ya mipaka huku akisisitiza “naomba mshirikiane nao.”

Rais Magufuli amewataka wananchi wa Nkasi kulima kwa ili kuitendea haki ardhi waliyopewa kwa ajili ya shughuli hiyo “sasa naombeni mlime kweli,” amesema na kuongeza; “nitakuja kuuliza mmezalisha kiasi gani?”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!