Friday , 19 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Josephat Isango kuzikwa Jumanne
Habari Mchanganyiko

Josephat Isango kuzikwa Jumanne

Josephat isango
Spread the love

MWILI wa aliyekua Mwandishi wa habari Josephat Isango unatarajiwa kuzikwa siku ya Jumanne, saa nne asubuhi nyumbani kwao Kisasida mkoani Singida, anaandika Hamisi Mguta.

Marehemu Isango alifariki dunia jana mapema asubuhi katika hospitali ya Ikungi mkoani Singida ambapo alilazwa kwa wiki mbili akisumbuliwa na Kifua, hata hivyo uchunguzi wa afaya yake ul;ibainisha ana tatizo la kupanuka kwa moyo.

Enzi za uhai wake, Marehemu alifanya kazi katika kampuni mbalimbali ikiwemo Free Media wazalishaji wa magazeti ya Tanzania Daima na Sayari pia aliwahi kufanya kazi katika kampuni ya Hali Halisi Publishers wazalishaji wa magazeti ya Mawio na MwanaHALISI.

Mwandishi huyo ambaye alisifika kwa ujasili wake katika kutetea haki za wanyonge, Mwaka 2015 aliwahi kukumbwa na tukio la kushambuliwa na polisi wa FFU eneo la mbele ya makao makuu ya Jeshi la Polisi katikati ya jijini Dar es Salaam alipokuwa na waandishi wengine wakisubiri kuwasili kwa viongozi wakuu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).

Aliwahi kuugua akiwa jijini Dar es Salaam na baada ya muda mfupi aliamua kusafiri kwenda Singida, mkoa wa nyumbani kwao ndipo mauti yakamkuta.

 

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

NEMC yaonya wanaojenga bila tathmini ya mazingira

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC),...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

Habari Mchanganyiko

Carbon First, Ruangwa wasaini makubaliano ya biashara ya hewa ukaa

Spread the love  KAMPUNI ya Carbon First Tanzania Limited na Halmashauri ya...

Habari Mchanganyiko

CBE yawakumbuka wenye mahitaji maalum Jangwani

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimetoa msaada mbalimbali na...

error: Content is protected !!