Monday , 11 December 2023
Home Gazeti Habari za Siasa JKT wakabidhiwa kiwanda cha korosho Lindi
Habari za Siasa

JKT wakabidhiwa kiwanda cha korosho Lindi

Baadhi ya sehemu ya mtambo ya kiwanda cha Korosho cha Buko, mkoani Lindi
Spread the love

BAADA ya Serikali kukitwaa kiwanda cha kuchakata korosho kilichopo mkoani Lindi Buko, Rais John Magufuli amekikabidhi kiwanda hicho kwa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT). Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Akizungumza leo tarehe 12 Novemba 2018 Ikulu jijini Dar es Salaam, Rais Magufuli amesema kiwanda hicho kitakuwa chini ya JKT na kwamba endapo jeshi hilo litashindwa kukiendesha, litanyang’anywa na kukabidhiwa kwa watu wengine.

Katika hatua nyingine, Rais Magufuli ameagiza korosho zitakazonunuliwa na serikali, kiasi zipelekwe kwenye kiwanda cha Buko.

“Korosho hizo zikinunuliwa jeshi litapeleka kwenye magodauni, hiyo korosho itakayosombwa itapelekwa nyingine kwenye kiwanda cha Buko mkoani Lindi, kiwanda hiki nimewapa wanajeshi JKT mpaka hapo kikiwashinda kukitumia tutawanyang’a, tutakipeleka kwa watu wengine,” amesema Rais Magufuli.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Jaji Kiongozi akerwa wananchi kukosa imani na mahakama

Spread the loveWATENDAJI wa Mahakama ya Tanzania, wametakiwa kuweka mikakati itakayosaidia kurejesha...

BurudikaHabari za Siasa

Samia amchangia Professa Jay mil. 50, Chadema, wasanii wamwaga manoti

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan amechangia kiasi cha Sh 50 milioni...

Habari za Siasa

Biteko: Samia ni muumini wa maridhiano sio kwa kuigiza

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Mpango: Sitakufa bali nitaishi

Spread the loveMAKAMU  wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk....

error: Content is protected !!