Wednesday , 17 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa JKT wakabidhiwa kiwanda cha korosho Lindi
Habari za Siasa

JKT wakabidhiwa kiwanda cha korosho Lindi

Baadhi ya sehemu ya mtambo ya kiwanda cha Korosho cha Buko, mkoani Lindi
Spread the love

BAADA ya Serikali kukitwaa kiwanda cha kuchakata korosho kilichopo mkoani Lindi Buko, Rais John Magufuli amekikabidhi kiwanda hicho kwa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT). Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Akizungumza leo tarehe 12 Novemba 2018 Ikulu jijini Dar es Salaam, Rais Magufuli amesema kiwanda hicho kitakuwa chini ya JKT na kwamba endapo jeshi hilo litashindwa kukiendesha, litanyang’anywa na kukabidhiwa kwa watu wengine.

Katika hatua nyingine, Rais Magufuli ameagiza korosho zitakazonunuliwa na serikali, kiasi zipelekwe kwenye kiwanda cha Buko.

“Korosho hizo zikinunuliwa jeshi litapeleka kwenye magodauni, hiyo korosho itakayosombwa itapelekwa nyingine kwenye kiwanda cha Buko mkoani Lindi, kiwanda hiki nimewapa wanajeshi JKT mpaka hapo kikiwashinda kukitumia tutawanyang’a, tutakipeleka kwa watu wengine,” amesema Rais Magufuli.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Samia arejesha mikopo ya 10%, bilioni 227.96 zatengwa

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amerejesha utaratibu wa utoaji mikopo...

Habari za Siasa

Rais Samia amfariji mjane wa Musa Abdulrahman

Spread the loveRais Samia Suluhu Hassan leo Jumanne amempa pole Mwanakheri Mussa...

Habari za Siasa

Nape: Wanasiasa, wanahabari, wafanyabiashara mteteeni Samia

Spread the loveWaziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari na Mawasiliano,...

Habari za Siasa

CAG: TAWA imegawa vibali vya uwindaji bila idhini ya waziri

Spread the loveRIPOTI ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali...

error: Content is protected !!