Monday , 5 June 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Jiji la Arusha lawaonya wanaoleta vurugu
Habari za Siasa

Jiji la Arusha lawaonya wanaoleta vurugu

Spread the love

HALMASHAURI ya Jiji la Arusha, limeonya kuwachukulia hatua za kisheria wanaojihusisha na mgogoro wa maduka yake yaliyopo eneo la standi ndogo, anaandika Mwandishi Wetu.

Onyo hilo lilitolewa na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, Athuman Kihamia, kuwa baadhi ya watu wanachangia kuleta vurugu kati ya halmashauri, wamiliki wa maduka na wapangaji.

Amesema mgogoro huo ulishakwisha miezi miwili iliyopita na kufikia makubaliano kwa pande zote tatu ili kutafuta suluhu ambayo imesaidia kuepusha hali ya uvunjifu wa amani na watu kufanya biashara kwa mujibu wa sheria na makubaliano waliyojiwekea.

Amesema kuna baadhi ya wapangaji ambao wanachochea mgogoro huo kutokana kukataa kulipa malimbikizo ya kodi za nyuma wanazodaiwa hivyo wanadai kuwa maridhiano yaliyofanyika awali hawayatambui.

Onyo la Kihamia linafuatia viongozi wa wafanyabiashara kuzungumza na vyombo vya habari mwishoni mwa wiki iliyopitia wakimwomba Rais John Magufuli kusikiliza kilio chao na kuwasaidia kutatua mgogoro huo uliodumu kwa muda mrefu.

Walidai muda wa miezi miwili hadi sasa maduka yao yamefungwa na watu wanaojiita wawekezaji wajenzi ambao wamewaamuru kuondoka.

Akizungumza kwa niaba ya wafanyabiashara hao mwenyekiti wa wafanyabiashara wapangaji, Josephine Shirima, alisema mnamo Mei mwaka huu, watu waliojitambulisha kuwa ni wamiliki wa maduka hayo walifika majira ya usiku na kufunga maduka yao kwa sababu ambazo hazijawekwa wazi hadi sasa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Lusinde: CCM hatuliachii ng’o jimbo la Moshi Mjini

Spread the loveMJUMBE wa Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (NEC), Livingston...

Habari za SiasaTangulizi

Serikali ya Mapinduzi Zanzibar: Bakharesa hajavamia shamba letu

Spread the love  IKULU Visiwani Zanzibar, imeeleza kuwa eneo la kiwanda cha...

Habari za SiasaTangulizi

Zanzibar watangaza rasmi kuwa shamba la Razaba ni mali yao

Spread the love  SERIKALI ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), imetangaza rasmi kwamba shamba...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Mwinyi azindua Kamati ya Maridhiano Visiwani

Spread the love  RAIS wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), Dk. Hussein...

error: Content is protected !!