Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Jibu la hekima la Prof. Assad
Habari za SiasaTangulizi

Jibu la hekima la Prof. Assad

Aliyekuwa Mdhibiti na Mkaguzi wa Hesabu za Serikali (CAG), Prof. Assad Mussa (kulia) akimkaribisha CAG mpya, Charles Kichere ofisi muda mchache kabla ya kumkabidhi ofisi hiyo
Spread the love

PROFESA Mussa Assad, aliyekuwa Mdhibiti na Mkaguzi wa Hesabu za Serikali (CAG), anatarajiwa kukabidhi ofisi leo tarehe 5 Novemba 2019. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Hata hivyo, amesema ‘sina kinyongo’ baada ya kuhojiwa na vyombo mbalimbali vya habari kuhusu ‘kustaafishwa’ kwake kwa mujibu wa Ikulu, jijini Dar es Salaam.

“Kwa kuwa nimefanya kazi kwa uadilifu, nadhani kusamehe ni bora zaidi, sina kinyongo. Sijawahi kabisha kumtengenezea mtu maudhi, sasa najiandaa kufuga kuku,” amesema Prof. Assad alizungumza tarehe 4 Novemba 2019 .

Mtaalamu huyo mbobezi katika masuala ya ukaguzi, alitenguliwa kwenye nafasi hiyo na Rais John Magufuli tarehe 3 Novemba 2019, kabla ya kupewa barua ya utenguzi huo.

Taarifa ya kutenguliwa kwake ilitangazwa na Balozi John Kijazi, Katibu Mkuu Kiongozi ambapo ilieleza, Charles Kichere kuchukua nafasi hiyo.

Leo tarehe 5 Novemba 2019, Prof. Assad amekutana na Kichere na kukabidhi taasisi na kwamba, makabidhiano rasmi yatafanyika Dodoma.

“Mimi nimepokea ofisi hii kutoka kwa bwana Uttoh (Ludovick Uttoh) five years ago (miaka mitano iliyopita), naamini sikufanya energy destructions (uharibifu).

“Mimi huwa naamini changes (mabadiliko) zinaweza kutokea, lakini zitokee kwa namna zilivyopangwa vizuri, si mwaminifu wa kutoa watu wote and then (halafu) unaweka new team (watu wapya),” amesema Prof. Assad wakati wa makabidhiano hayo ya awali.

Awali, akizungumza namna alivyoshirikiana na watumishi wengine Prof. Assad alisema, hana kumbukumbu ya kumtendea uovu mtu yeyote kwa kudhamiria katika maisha yake, na kwamba huwenda kuna watu walioteseka kwa kutenda uadilifu.

Alieleza kuwahi kuwaachisha kazi wafanyakazi wanne kutokana na wizi, na kwamba ilikuwa hitajio la kisheria kwa kuwa waliofukuzwa walikutwa na hatia.

Prof. Assad aliyeingia kwenye nafasi hiyo baada ya kuteuliwa na Rais Jakaya Kikwete tarehe 1 Desemba 2014 amesema, hatofanya kazi yoyote serikali kwa kuwa, Katiba ya Jamhuri inazuia CAG kufanya kazi yoyote serikalini baada ya kuondoka mamlakani.

Akifafanua zaidi, CAG amesema anajiandaa kwenda kufuga kuku sambamba na kuendeleza kilimo. Amesema, “sasa nakwenda kufuga kuku na kulima, tuna mashamba makubwa.”

Prof. Assad (58) aliondolewa madarakani tarehe 3 Novemba 2019, akiwa kwenye mkutano wa sita wa Taasisi za Fedha za Kiislamu barani Afrika.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia ataja mikakati ya kufikia trilioni 2 biashara Uturuki, Tz

Spread the loveWakati Tanzania na Uturuki zikidhamiria kuongeza kiwango cha biashara hadi...

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

Habari za Siasa

Wabunge waikalia kooni TAKUKURU Bungeni

Spread the love  BAADHI ya wabunge wamelia na changamoto za utendaji wa...

error: Content is protected !!