Wednesday , 6 December 2023
Home Habari Mchanganyiko Jeshi la Tanzania lataka wananchi waishio porini kuondoka
Habari Mchanganyiko

Jeshi la Tanzania lataka wananchi waishio porini kuondoka

Spread the love

JESHI la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), limewataka raia kuondoka porini karibu na mpaka wake na taifa la Msumbiji, wakati huu wanapojiandaa kupambana na wanamgambo waliojipachika jina la “wapiganaji wa kiislamu.” Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Mkuu wa operesheni hiyo alisema, jeshi litaanza kuwatafuta wahalifu katika pori la Ruvuma, na baadaye Mtwara na Lindi.

Taarifa kwamba serikali ya Tanzania imepanga kutumia majeshi yake kufanya “operesheni maalum” katika mpaka wake na Msumbiji, zinakuja katika kipindi ambacho serikali ya Marekani imetahadharisha kuwapo makundi ya kihalifu katika eneo hilo.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, wanamgambo hao wanafanya operesheni zao eneo la Kaskazini la Msumbiji, liitwalo Cabo Delgado, huku wakiungwa mkono na wanamgambo wa Islamic State.

Mkuu wa operesheni maalum ya Marekani barani Afrika, Meja Jenerali Dagvin Anderson, amewaambia waandishi wa habari kuwa kundi hilo limekuwa likipata msaada kutoka nje, hali inayolifanya kuwa hatari zaidi.

Wanamgambo hao wanadaiwa kushambulia vijiji mbalimbali katika kipindi cha miaka miwili iliyopita.

Alisema, “tumewashuhudia katika kipindi cha miezi 12 mpaka 18 wakiimarisha uwezo wao wa mashambulizi, na kutumia mbinu ambazo hutumika pia katika maeneo mengine ya ulimwengu, hasa Mashariki ya Kati ambako kuna makundi yenye uhusiano na Islamic State.”

Uasi wa wanamgambo wa kiislamu waliojitokeza katika kona ya mbali za Msumbiji umegeuka kuwa vita vya wazi katika wiki za hivi karibuni.

Ripoti za mauaji ya watu, kukatwa kichwa na kutekwa nyara kwa miji miwili katika mkoa wa Cabo Delgado, ni vitendo ambavyo vimekuwa vikiripotiwa kila siku, aliandika mwandishi wa BBC Africa, Andrew Harding.

Me mwaka huu, Tanzania ilipeleka majeshi yake katika mikoa hiyo ya mpakani baada ya kuibuka kwa shambulio la lililotekelezwa na wapiganaji wa kiislamu.

Taarifa zinasema, wapiganaji hao tayari wamevamia miji kadhaa na kuua mamia ya watu na maelfu kuhama makazi yao.

Picha za video, zilizopigwa Aprili mwaka huu kwa simu ya mkononi, wilayani Muidumbe zilikuwa ni ushahidi wenye nguvu kuwa mzozo uliokuwa gizani katika eneo hilo la Kaskazini mwa taifa hilo la Kusini Mashariki mwa AfrikaMsumbiji.

Aidha, picha nyingine za video zilizopigwa katika eneo la bandari Mocimboa da Praia, ambalo lilidhibitiwa kwa muda na wanamgambo tarehe 24 Machi, zinaonyesha wanamgambo hao walidhibiti mji mwingine muhimu wa Quissanga.

‘’Sasa wana silaha na magari, yanayowafanya waweze kutembea kirahisi na kufanya mashambulizi kwenye eneo kubwa. Na hutumia sare za wanajeshi. Hivyo, watu huchanganyikiwa na kuogopa,” anasema Askofu wa kikatoliki wa Pemba, Luiz Fernando Lisboa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Shura ya Maimamu kukata rufaa kupinga Sheikh kufungwa miaka 7

Spread the loveSHURA ya Maimamu Tanzania, inakusudia kukata rufaa dhidi ya hukumu...

Habari Mchanganyiko

TMA yaagizwa kutangaza mafanikio yao kikanda, kimataifa

Spread the love  KATIBU Mkuu Wizara ya Uchukuzi, Prof. Godius Kahyarara ameiagiza...

Habari Mchanganyiko

NMB yasaidia waathirika wa mafuriko, maporomoko Hanang

Spread the loveWaathirika wa maporomoko ya tope Wilayani Hanang, mkoani Manyara, waliopoteza...

Habari Mchanganyiko

TPF-NET Arusha yaonya jamii ya wafugaji zinazoendeleza ukatili wa watoto na wanawake

Spread the love  MTANDAO wa Polisi wanawake wa Arusha kuelekea siku 12...

error: Content is protected !!