Saturday , 25 March 2023
Home Kitengo Michezo Jeshi la Polisi latoa tahadhari Simba na Yanga
Michezo

Jeshi la Polisi latoa tahadhari Simba na Yanga

Spread the love

 

 JESHI la Polisi kanda maalumu ya Dar es Salaam limesema kuwa limejipanga kuimalisha ulinzi, kwenye mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara kati ya Simba na Yanga utakaopigwa kwenye dimba la Benjamin Mkapa. Anaripoti Kelvin Mwaipungu…(endelea)

Mchezo huo utaanza majira ya saa 11 jioni, Tarehe 3 Julai 2021, ambapo klabu ya Simba ndio watakaokuwa wenyeji wa mchezo.

Taarifa kutoka ndani ya jeshi hilo imeeleza kuwa, wamejiapanga kuweka Askari wa kutosha katika kila eneo ndani ya Uwanja huo.

Mechi hiyo ambayo inavuta hisia za mashabiki wengi wa mchezo huo nchini, kutokana na ukubwa wa klabu hizo ndani ya Tanzania.

Aidha Polisi wametoa zuio kwa mashabiki kuingia Uwanjani na chupa ya Maji au kinywaji chochote, silaha pamoja na mashabiki kukaa sehemu ambapo tiketi zao haziwaruhusu.

Pia jeshi la polisi limetoa tahadhari kwa watakao kwenda na watoto Uwanjani, kuwanao karibu au kutumia busara kwa kuwaacha nyumbani.

Huu utakuwa mchezo wa kufunga dimba kwenye mzunguko wa Pili wa Ligi Kuu Tanzania Bara, kwa msimu wa 2020/21, kwenye mchezo wa kwanza timu hizo zilitoka kwa kufungana bao 1-1.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Yanga: Fedha za Rais Samia zinaleta ari kubwa

Spread the loveUONGOZI wa klabu ya Yanga, umesema fedha zinazotolewa na Rais...

Michezo

Simba Sc. yamvulia kofia Rais Samia, yamuahidi makubwa dhidi ya Horoya

Spread the loveWAKATI timu ya Simba ikiibuka na ushindi wa bao 3-0...

Michezo

Taasisi ya TKO na TFF yawapiga msasa makocha wa kike 54

Spread the love WAKATI Soka la wasichana likichipua kwa kasi Taasisi ya...

Michezo

Kimwanga CUP yazidi kutimua vumbi

Spread the loveMASHINDANO ya mpira wa miguu ya Kimwanga CUP ya kuwania...

error: Content is protected !!