Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari Jeshi la Polisi latoa masharti matano mchezo Simba na Yanga
HabariMichezo

Jeshi la Polisi latoa masharti matano mchezo Simba na Yanga

Spread the love

 

JESHI la Polisi kanda maalumu ya Dar es Salaam limetoa masharti matano kuelekea mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara kati ya Simba na Yanga ikiwemo kutaka mashabiki kuepuka mihemko ya maneno ya kuhasimiana wakati mchezo huo unaendelea. Anaripoti Kelvin Mwaipungu…(endelea)

Mchezo huo utafanyika siku ya Jumamosi majira ya saa 11 jioni kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es salaam.

Akiongea mbele ya waandishi wa Habaru hii leo Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa amesema kuwa jeshi hilo limejipanga kuimalisha ulinzi siku ya mchezo huo katika maeneo yote ya Uwanja zikiwemo barabara za kuingia na kutoka Uwanjani hapo sambamba na kutoa masharti kwa mashabiki watakaokwenda kuangalia mchezo huo.

Kamanda wa Polisi, Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa

 

“Hatutaruhusu mashabiki kuingia na chupa za maji uwanjani kwa kuwa hutumiwa kurushiana pale timu moja inapokuwa haikubali matokeo sambamba na kutoruhusu kuingia na Silaha ambayo inaweza kugeuka kuwa hatari” alisema Mambosasa

“Hatutoruhusu kupaki magari ndani ya Uwanja na magari yatakayo ruhusiwa ni yenye vibari maalumu na pia hatutoruhusu kukaa sehemu ambao tiketi yako haikuruhusu kukaa naomba uheshimu hali yako” alisema Kamanda huyo

https://www.youtube.com/watch?v=2WXuOcNZRBA

Aidha jeshi hilo limetoa tahadhari kwa wazazi watakaokwenda na watoto Uwanjani siku ya mchezo huo kuwa makini na kujiepusha kukaa sehemu zenye msongamano.

Mchezo huu unakutanisha timu ambazo zipo juu kwenye msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara, ambapo Simba ipo kwenye nafasi ya kwanza ikiwa na pointi 61 mara baada ya kucheza michezo 25, huku nafasi ya pili wakiwa Yanga wenye pointi 57 mara baada ya kucheza michezo 27.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Makala & UchambuziMichezo

TFF kuamua hatima ya Amrouche

Spread the loveHATIMA ya Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Adel Amrouche kuendelea...

Habari za SiasaMichezo

Matinyi: Dk. Ndumbaro alifanya utani ukaguzi mechi za Yanga, Simba

Spread the loveMsemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi amesema kauli iliyotolewa na...

Michezo

Gethsemane Group Kinondoni (GGK) waachia video ya Bwana Wastahili

Spread the loveWAIMBAJI maarufu nchini kutoka Gethsemane Group Kinondoni (GGK)SDA wameachia video...

BiasharaMichezo

Gamondi kocha bora mwezi Februari, NBC yamjaza manoti

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambae ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!