Friday , 29 September 2023
Home Kitengo Habari Kimataifa Jeshi kumfungulia mashtaka rais kwa uhaini
Kimataifa

Jeshi kumfungulia mashtaka rais kwa uhaini

Rais wa Niger, Mohamed Bazoum
Spread the love

VIONGOZI wa mapinduzi ya kijeshi nchini Niger wametangaza kuwa na ushahidi wa kumshtaki rais aliyeondolewa madarakani na washirika wake wa ndani na nje kwa uhaini mkubwa pia kwa kuhatarisha usalama wa ndani na nje wa Niger. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa …(endelea).

Rais wa Niger, Mohamed Bazoum ambaye aliondolewa madarakani na kuzuiliwa tangu tarehe 26 Julai 2023 baada ya mapinduzi yaliyoongozwa na wanajeshi, anakabiliwa na shutuma mpya kutoka kwa jeshi hilo.

Jeshi ambalo liliunda serikali katika kipindi hiki cha machafuko nchini Niger, jana Jumapili limetangaza kwamba wana nia ya kumshtaki mkuu huyo wa nchi aliyeondolewa mamlakani kwa uhaini na kwa kuhatarisha usalama wa nchi.

Kanali Meja Amadou Abdramane ambaye ni mmoja wa wajumbe wa serikali, katika taarifa kwa vyombo vya habari iliyosomwa kwenye televisheni ya taifa imebainisha kuwa rais huyo anayezuiliwa alirekodiwa njia ya simu.

Mohamed Bazoum, familia yake na washirika wake kadhaa wa karibu bado wanazuiliwa katika chumba cha chini cha makazi ya rais huko Niamey.

Siku ya Jumamosi tarehe 12 Agosti 2023, rais wa Niger alitembelewa na daktari wake wa kibinafsi.

Kulingana na daktari huyo, wote wanaozuiliwa wanaendelea vyema na Mohamed Bazoum naye iko vizuri kiafya.

Hata hivyo, Rais Bazoum alisema kuwa matibabu yaliyotengwa kwa ajili ya familia yake na yeye mwenyewe ni ya kinyama na ya kikatili.

Jana Jumapili, mamlaka ya kijeshi pia ilishutumu vikwazo haramu, vya kinyama na vya kufedhehesha vilivyowekwa na Jumuiya ya Kiuchumi ya Nchi za Afrika Magharibi (ECOWAS), ambayo inapinga mapinduzi hayo na kutishia kuivamia nchi hiyo ili kurejesha utawala wa kikatiba, ingawa njia ya diplomasia inapendekezwa kila wakati.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Kimataifa

Wadukuzi wa Kichana waiba barua pepe 60,000 za Serikali ya Marekani

Spread the loveWADUKUZI wa kichana wamedukua barua pepe 60000 serikali ya Marekani...

Kimataifa

Mahakama yamkuta na hatia Donald Trump

Spread the love  ALIYEKUWA Rais wa Marekani, Donald Trump, amekutwa na hatia...

Kimataifa

Harusi yageuka msiba 100 wakifariki kwa ajali ya moto

Spread the love  WATU takribani 100, akiwemo bibi na bwana harusi, wamefariki...

Kimataifa

Kampuni ya mali ya China Oceanwide yapata agizo la kufilisiwa huko Bermuda

Spread the love  MAHAKAMA ya Bermuda imetoa amri ya kufilisiwa kwa Kamapuni...

error: Content is protected !!