Saturday , 20 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Jeshi kukabiliana na wafuasi wa Zuma
Kimataifa

Jeshi kukabiliana na wafuasi wa Zuma

Wafuasi wa Jacob Zuma
Spread the love

 

SERIKALI ya Afrika Kusini imelazimika kuingiza Jeshi mtaani, ili kutuliza ghasia zilizoanzishwa na wafuasi wa rais mstaafu wa nchi hiyo, Jacob Zuma (79), wakipinga mwanasiasa huyo kufungwa miezi 15 gerezani. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).

Ghasia hizo ziliibuka jana tarehe 12 Julai 2021, katika Mkoa wa Gauteng na KwaZulu –Natal, mkoa anaotoka Zuma, ambapo wafuasi hao walivamia baadhi ya maduka na kuchoma majengo kadhaa.

Tangu mwanasiasa huyo ajisalimishe gerezani wiki iliyopita, watu sita wamefariki dunia kutokana na ghasia hizo, huku 500 wakiamatwa.

Wafuasi hao waliingia mitaani na kuanza kufanya fujo, mara baada ya kesi ya Zuma kusikilizwa katika Mahakama ya Kikatiba nchini humo, bila mafanikio kwa mwanasiasa huyo, ambaye alitarajia kupewa dhamana au kupunguziwa adhabu yake.

Jacob Zuma

Rais wa Afrika Kusini, Cyril Ramaphosa, aliwaomba wananchi wasijihusishe na ghasia hizo, huku akiwalaani waliozianzisha.

Zuma alihukumiwa kifungo hicho na Mahakama ya Kikatiba nchini humo, baada ya kubainika na hatia katika kosa la kuidharau mahakama hiyo, kufuatia hatua yake ya kutohudhuria mahakamani kusikiliza kesi ya ufisadi inayomkabili.

Rais huyo wa zamani wa Afrika Kusini, anatuhumiwa kufanya makosa ya ufisadi alipokuwa madarakani, lakini mara kadhaa amekana makosa hayo.

Zuma alikuwa Rais wa Afrika Kusini kwa miaka tisa mfululizo, kuanzia 2009 hadi 2018.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!