Tuesday , 26 September 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Jerry Silaa awageukia wakuu wa mikoa migogoro ya ardhi
Habari za Siasa

Jerry Silaa awageukia wakuu wa mikoa migogoro ya ardhi

Spread the love

WAZIRI wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Jerry Silaa amewataka wakuu wa mikoa kutekeleza maagizo yaliyotolewa na kamati ya mawaziri nane, kwa ajili ya kutatua migogoro ya ardhi katika maeneo yao. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma…(endelea).

Silaa ametoa agizo hilo leo tarehe 6 Septemba 2023, bungeni jijini Dodoma, akijibu swali la Mbunge Viti Maalum, Condester Sichalwe, lililohoji mpango wa serikali katika kumaliza migogoro ya ardhi iliyoko katika Kata ya Kapele, mkoani Songwe.

“Serikali imepinga na  Serikali kupitia kamati ya mawaziri nane ilishafanya utatuzi wa migogoro ya ardhi kwenye vijiji 975 na naomba kutumia fursa hii kuwakumbusha wakuu wa mikoa nchi nzima kuendelea na utekelezaji wa maagizo ya baraza la mawaziri,” amesema Silaa.

Mbali na agizo hilo, Silaa amesema atafanya ziara nchi nzima ili kuhakikisha maagizo ya kamati hiyo ya mawaziri yanafanyiwa kazi.

Awali, Sichalwe akiuliza swali lake alisema “lini wizara itaingia kati na kutusaidia migogoro ya ardhi iliyoko ndani ya Kata ya Kapele? Kwa kufuatilia watu wamehodhi na kupora maeneo ya wananchi kinyume na taratibu na wengine kuwa na hati za uongo kwa kigezo wameagizwa na wakubwa huko juu.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Rais Samia avunja bodi ya REA

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amemteua Balozi Jacob Kingu, kuwa...

Habari za SiasaTangulizi

Chande aliyeng’olewa TANESCO kwenda TTCL apelekwa Posta

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amemteua aliyekuwa, Mkurugenzi Mkuu wa...

Habari za Siasa

Kamugisha aanika utekelezaji mpango kazi 2022/23

Spread the loveMWENYEKITI wa Ngome ya Vijana ya Chama Cha ACT-Wazalendo Mkoa...

Habari za Siasa

Vijana ACT-Wazalendo wakabidhiwa kivumbi kulinda kura uchaguzi 2024,2025

Spread the loveNGOME ya Vijana ya Chama cha  ACT-Wazalendo, imetakiwa kuwanoa wafuasi...

error: Content is protected !!