Friday , 19 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Jenerali Mabeyo:Vita ya ugaidi ngumu
Habari MchanganyikoTangulizi

Jenerali Mabeyo:Vita ya ugaidi ngumu

Spread the love

 

MKUU wa Majeshi ya Ulinzi nchini, Jenerali Venance Mabeyo, amewaomba wananchi watoe ushirikiano kwa vyombo vya ulinzi na usalama katika kukabiliana na ugaidi kwa kuwa vita hiyo ni ngumu. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Jenerali Mabeyo ametoa kauli hiyo leo Jumamosi, tarehe 27 Novemba 2021, jijini Dodoma wakati akitoa taarifa ya mafanikio na changamoto za Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), ndani ya miaka 60 ya uhuru wa Tanzania Bara.

Mkuu huyo wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania, amesema vita hiyo ni ngumu kutokana na mbinu zinazotumiwa na magaidi kuwa si rahisi kuwatambua kutokana na kujigawa katika vikundi vidogo vidogo.

“Vita hii ni ngumu, inahitaji umakini mkubwa kwa sababu mbinu wanazotumia katika mapigano hayo sio ule utamaduni wa mapigano ya kawaida, wanapigana katika vikundi vidogo vidogo,” amesema Jenerali Mabeyo.

Jenerali Mabeyo amesema, viashiria vya ugaidi vipo huku akikumbushia tukio la mauaji ya wananchi katika wilaya ya Kibiti mkoani Pwani.

“Tunayo matishio mengi kutoka nje lakini tunayo ndani, viashiria vya ugaidi vipo. Vilevile nchini kwetu na hivi naamini nyie ni walewa wakubwa, ni vita ambayo imeanzia mataifa mengine na inasogea, imekuja mpaka kwetu,” amesema Jenereli Mabeyo.

Jenerali Mabeyo amesema “kama mnakumbuka ilianzia mbali, tuliona mkoani Tanga maeneo ya Amboni, wakateremka wakaja Kibiti, kama mtakumbuka maeneo ya Kibiti, Mkuranga tulipambana kidogo na wakateremka Kusini tukapambana nao kule Mtwara na Ruvuma wakavuka mipaka wengine ndiyo sasa unawasikia wako Msumbiji.”

Jenerali Mabeyo amesema, kazi wanayoifanya sasa ni kuhakikisha wanadhibiti hali hiyo kwa kushirikiana na wananchi.

“Lakini kazi kubwa inayofanyika kuhakikisha tunadhibiti hali hiyo na msaada mkubwa lazima utoke kwa wananchi, ndiyo wanaoishi na vikundi hivi. Wako miongoni mwetu bila kufichuliwa na wananachi JWTZ haiwezi kukabiliana nao,” amesema Jenerali Mabeyo na kuongeza:

Jenerali Mabeyo amesema “ulinzi ni wa Watanzania wote, kila mahali ulipo matukio unayaona vishirikishe vyombo vya ulinzi na usalama ili viweze kukabiliana nao hasa mbinu wanazotumia mara nyingine wanastukiza.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Habari za SiasaTangulizi

Tanzania, Uturuki zanuia kukuza biashara, uwekezaji

Spread the loveSERIKALI za Tanzania na Uturuki zimekubaliana kuendeleza dhamira ya kuimarisha...

error: Content is protected !!