Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa January amshukuru Rais Samia, aahidi kupiga kazi kivitedo
Habari za Siasa

January amshukuru Rais Samia, aahidi kupiga kazi kivitedo

Spread the love

 

JANUARY Makamba, Waziri wa Nishati nchini Tanzania, ametoa shukrani kwa wote waliompongeza kwa kuteuliwa kuwa waziri na kuwaahidi kuwatumikia kwa vitendo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Makamba ambaye ni Mbunge wa Bumbuli (CCM), ametoa pongezi hizo baada ya juzi Jumatatu, tarehe 13 Septemba 2021, Ikulu ya Chamwino Dodoma, kuapishwa kuwa waziri wa nishati.

Amechukua nafasi ya Dk. Merdard Kalemani, Mbunge wa Chato ambaye uteuzi wake umetenguliwa.

Katika ukurasa wake wa Twitter, Makamba aliyewahi kuwa Waziri wa Muungano na Mazingira ameandika “nawashukuru nyote mlionitumia ujumbe wa pongezi na kunitakia heri. Sio kazi nyepesi lakini nitajitahidi.”

“Namshukuru Mhe Rais @SuluhuSamia kwa imani aliyoionyesha kwangu. Sitamuangusha. Katika wiki zijazo, tutaonyesha kwa vitendo umuhimu wa sekta hii kwa mustakabali wa nchi.”

Mbali na kuwa waziri wa Muungano na Mawasiliano, Makamba amewahi kuwa naibu waziri wa mawasiliano, sayansi na teknolojia.

1 Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!