Tuesday , 21 March 2023
Home Gazeti Habari za Siasa January amshukuru Rais Samia, aahidi kupiga kazi kivitedo
Habari za Siasa

January amshukuru Rais Samia, aahidi kupiga kazi kivitedo

Spread the love

 

JANUARY Makamba, Waziri wa Nishati nchini Tanzania, ametoa shukrani kwa wote waliompongeza kwa kuteuliwa kuwa waziri na kuwaahidi kuwatumikia kwa vitendo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Makamba ambaye ni Mbunge wa Bumbuli (CCM), ametoa pongezi hizo baada ya juzi Jumatatu, tarehe 13 Septemba 2021, Ikulu ya Chamwino Dodoma, kuapishwa kuwa waziri wa nishati.

Amechukua nafasi ya Dk. Merdard Kalemani, Mbunge wa Chato ambaye uteuzi wake umetenguliwa.

Katika ukurasa wake wa Twitter, Makamba aliyewahi kuwa Waziri wa Muungano na Mazingira ameandika “nawashukuru nyote mlionitumia ujumbe wa pongezi na kunitakia heri. Sio kazi nyepesi lakini nitajitahidi.”

“Namshukuru Mhe Rais @SuluhuSamia kwa imani aliyoionyesha kwangu. Sitamuangusha. Katika wiki zijazo, tutaonyesha kwa vitendo umuhimu wa sekta hii kwa mustakabali wa nchi.”

Mbali na kuwa waziri wa Muungano na Mawasiliano, Makamba amewahi kuwa naibu waziri wa mawasiliano, sayansi na teknolojia.

1 Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Rais Samia aagiza iundwe kamati ya pamoja ya Mawaziri mradi wa BBT

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amewaagiza mawaziri kuunda kamati...

Habari za Siasa

Rais Samia apangua makatibu tawala mikoa, ateua Kamishna DCEA

Spread the loveALIYEKUWA Kamishna wa Mamlaka ya Kudhibiti Dawa za Kulevya, Gerald...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

M/kiti bodi ya wadhamini Chadema afariki dunia

Spread the loveMWENYEKITI wa Bodi ya Wadhamini ya Chama cha Demokrasia na...

Habari za Siasa

Zitto: Nikifa Ado atavaa viatu vyangu

Spread the love  KIONGOZI Mkuu wa Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe...

error: Content is protected !!